logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wewe ni wa baraka-Betty Kyallo asherehekea siku ya kuzaliwa ya mwanawe kwa ujumbe maalum

Kulingana na Betty mwanawe ni baraka kwake na kwa familia yake.

image
na Radio Jambo

Habari22 June 2022 - 09:01

Muhtasari


  • Ni furaha ya kila mzazi kumuona mwanawe au wanawe wakikua kila kuchao, na hata kuendelea na maisha yao
Instagram, KWA HISANI

Mwanahabari na mjasirimali Betty Kyallo sio mgeni vinywani mwa wengi au kwenye mitandao ya kijamii.

Betty amekuwa akifahamika sana kutokana na bidii ya kazzi yake, na kupiga hatua moja hadi nyingine ya maisha na biashara yake.

Pia anafahamika kutokana na uhusiano wake wa kimapenzi, amapo hajakuwa akificha uhusiano wake kutoka kwa mashabiki.

Ni furaha ya kila mzazi kumuona mwanawe au wanawe wakikua kila kuchao, na hata kuendelea na maisha yao.

Betty amebarikiwa na mtoto mmoja ambaye anaadhimisha miaka 8 hii leo,huku akiwa mwenye furaha alimlimbiikizia sifa teele mwanawe anaposherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Kulingana na Betty mwanawe ni baraka kwake na kwa familia yake.

Pia alimtakia kila la kheri, na kumuomba Mungu amlinde katika maisha yake, na hatua anazozichukua kila siku.

"Binti yangu mpendwa Ivanna. Heri ya miaka 8 ya kuzaliwa. Unaleta furaha na furaha nyingi katika maisha yetu. Wewe ni baraka. Unapendwa sana nami, familia yako yote lakini jinsi inavyostaajabisha WEWE NI KIPENZI CHA MIUNGU. Nakupenda mpenzi. Umekusudiwa kwa kila kitu ambacho ni KUU! Niko hapa kukuona ukiangaza kila siku. Utakuwa na sherehe kubwa zaidi kwa sababu unastahili," Betty Aliandika.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved