logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mbarikiwe,'Akuku Danger na Sandra Dacha wawashukuru Wakenya kwa kufanya haya

Akuku alisema kulazwa hospitalini mara nyingi mwaka huu kumemdhoofisha kiakili, kifedha na kimwili.

image
na Radio Jambo

Habari23 June 2022 - 08:55

Muhtasari


  • Jumatano, Akuku alisema kulazwa hospitalini mara nyingi mwaka huu kumemdhoofisha kiakili, kifedha na kimwili
Sandra Dacha almaarufu kama Silprosa na mpenzi wake Akuku Danger

Chini ya saa 24, Wakenya na mashabiki wa mcheshi Akuku Danger wameonyesha upendo wao kwa mcheshi huyo baada ya kuchanga zaidi ya nusu milioni.

Hii ni baada ya mcheshi huyo kutoa wito kwa wakenya wamchangie baada ya kuzuiliwa hospitali kwa kutolipa bili ya Sh883,000.

Akuku amekuwa akipokea matibabu katika hospitali ya Nairobi West baada ya kulazwa takriban wiki mbili zilizopita.

Jumatano, Akuku alisema kulazwa hospitalini mara nyingi mwaka huu kumemdhoofisha kiakili, kifedha na kimwili.

Ameeleza kwamba ugonjwa wa Sickle Cell Anemia ambao alizaliwa nao ndio umekuwa ukimwathiri kiasi cha kulazwa.

"Imekuwa changamoto lakini bado ninashikilia. Msichoke na Mimi," Akuku aliwaomba Wakenya.

Kupitia kwenye ukurasa wa Sandra wa instaram amefichua kwamba wakenya wamechanga zaidi ya elfu mia tano, kwa saa 20,huku akiwashukuru kwa kitendo hicho.

"Elfu mia tano kwa saa 20,aki wakenya nyinyi nitasema nini," Alisema Sandra Dacha.

Akuku Danger naye alisema;

"Mbarikiwe."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved