logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msanii Size 8 afichua kwa nini hataweza kupata mimba tena

Size 8 alihitimisha kwa kusema kuwa hataweza kuzaa tena.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri25 June 2022 - 06:19

Muhtasari


  • Msanii wa nyimbo za injili Size 8 akiwa kwenye mahojiano ameeleza kwa nini hataweza kuwa mjamzito au kubeba ujauzito tena

Msanii wa nyimbo za injili Size 8 akiwa kwenye mahojiano ameeleza kwa nini hataweza kuwa mjamzito au kubeba ujauzito tena.

Akizungumza katika mahojiano na Nicholas Kioko, Size 8 alisema kuwa kwa sasa anasumbuliwa na shinikizo la damu na anapokuwa mjamzito, shinikizo hupanda.

Size 8 alisema kuwa ni Mungu tu kwamba aliweza kuzaa watoto wake wawili. Alisema ujauzito wa Wambo na Junior nusura umuue kwa sababu alikuwa na shinikizo la juu la damu

Alieleza jinsi shinikizo lilisababisha kifo cha mtoto wake wa tatu na pia kuendelea na kufichua kwamba alikuwa karibu kufa mnamo Machi alipokimbizwa hospitalini kwa sababu shinikizo lake. ilikuwa juu sana sana.

Size 8 alihitimisha kwa kusema kuwa hataweza kuzaa tena.

Kwa sasa msanii huyo amebarikiwa na watoto wawili,ambao aliwapata kwa shida.

Pia akiwa kwenye mahojiano hayo aliwahimiza wakristo waweze kupendana kwani hata biblia inasema Mungu ni upendo, na kuwasaidia wanyonge hasa wakati huu maisha yamekuwa magumu.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved