logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Bahati ajue siasa si kama kanisa, kama amepigwa, apigane pia, asikuwe analialia" - Ringtone

"Siasa inakuwa ni nani alipiga mwingine. Sasa kama yeye amepigwa juzi, na yeye aende ampige yule aliyempiga, lakini isiwe si ile kumpiga ya kuumiza,” - Ringtone.

image
na Radio Jambo

Habari09 July 2022 - 22:00

Muhtasari


• “Mimi nataka kumuambia Bahati ajue siasa si kanisa, siasa si muskiti, siasa si harusi. Siasa ni pahali pa kupigana" - Ringtone.

Wasanii Ringtone na Bahati

Ringtone, ambaye hatimaye ameamua kuwafuata wenzake bahati Kioko na Willy Paul kwenye miziki ya kidunia baada ya kuigura tasnia ya injili, sasa anatetea kilio alichokitoa mahakamani wakati anatoa Ushahidi dhidi ya mwanablogu Robert Alai ambaye alimpiga rungu ya kichwa mwaka jana katika barabara moja mtaani Kilimani, Nairobi.

Ringtone alijitetea kwa kusema kwamba yeye analia mara moja moja tu hali ya kuwa msanii Bahati huwa na mazoea ya kulia kila mara kama mtoto.

Bahati amekuwa akionekana katika matukio mbali mbali akitokwa na machozi tu, tukio la hivi karibuni likiwa ni lile pindi baada ya kushinda tikiti ya Jubilee kuwania ubunge Matahre lakini akanyimwa tikiti ile baada ya Jubilee kusema kwamba muungano wa Azimio-One Kenya ambao chama hicho ni mojawapo, wameafikiana kufanya kitu kinaitwa ‘zoning’ ili kuwaondoa wagombea wasiokuwa na nguvu na kuwaunga mkono wagombea wenye ushawishi mkubwa.

Bahati alilia hadharani tena mbele ya kamera za wanahabari huku akiteta kwamab amefanyiwa hujuma baada ya kutumia pesa na nguvu nyingi kufanya kampeni.

Ringtone ambaye amejiunga nao kwenye uwanja wa miziki ya kidunia sasa ametoa ushauri kwa Bahati huku akimwambia kwamba ni sharti ajue siasa si kama Sanaa ya injili. Ikumbukwe Ringtone aliwahi jaribu siasa mwaka wa 2012 ambapo aliwania ubunge Kitutu Masaba katika uchaguzi wa mpito lakini akashindwa na kuburura mkia.

“Mimi nataka kumuambia Bahati ajue siasa si kanisa, siasa si muskiti, siasa si harusi. Siasa ni pahali pa kupigana. Siasa inakuwa ni nani alipiga mwingine. Sasa kama yeye amepigwa juzi, na yeye aende ampige yule aliyempiga, lakini isiwe si ile kumpiga ya kuumiza,” alitoa ushauri Ringtone.

Ringtone alisisitiza kwamba kwa kupiga hana maana ya vita bali ile kuweka watu wake pamoja ili kupiga kelele kwa kutamka jina lake na kumshinda mpinzani wake mwenye alikuwa na wafuasi wengi waliompigia kelele.

Ringtone alisema kwamab yeye aliamua kutumikia Wakenya wote badala ya kugombea kiti cha ubunge kwa sababu nafasi hiyo inakufunga kwa eneo moja tu lakini kwa muziki ni Wakenya wote wanaufikia muziki huo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved