logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Kwani Nandy ni benki?" Billnass ajibu madai kwamba alifuata Nnandy juu ya pesa na wala si mapenzi

“Kwani Nandy ni benki? Mtu akiona Nandy ana pesa sana hiyo ina maana huyo ni maskini sana kwa sababu mimi sijawahi ona Nandy kama ana pesa sana,” - Billnass.

image
na Radio Jambo

Habari13 July 2022 - 12:39

Muhtasari


• Billnass alisema yeye hajawahi muona Nandy kama mtu mwenye pesa na kusema tatizo lipo kwa wenye wanamuona hivo.

Wasanii na ambao pia ni wachumba, Billnass na Nandy

Msanii na mjasiriamali wa kampuni ya kuuza vifaa vya umeme ya Nengatronix, Billnass amekanusha vikali madai kwamba aliingia katika mahusiano na mwanamuziki Nandy kwa ajili ya utajiri wa malkia huyo wa muziki.

Akizungumza na wakuza maudhui wa mitandaoni, Nenga kama anavyojiita alisema hawezi mwambie mtu anayesema chochote kwa sababu siku zote wenye midomo lazima tu wataongea kwa sababu hiyo ndio kazi ya mdomo haswa.

“Kwani Nandy ni benki? Mimi sina chochote cha kumwambia mtu anayesema chochote kwa sababu kila mtu ana huru wa kusema kile anachofikiri kwa namna yake. Pia mtu akiona Nandy ana pesa sana hiyo ina maana huyo ni maskini sana kwa sababu mimi sijawahi ona Nandy kama ana pesa sana,” Billnass alisema.

Msanii huyo pia alisisitizac kwamba tatizo lipo kwa yule anayeliona hivyo kutokana na kipato chake kwani yeye hawezi eti ameacha mambo yake yote na kuanza kumfuata mwanamke kwa sababu ya pesa na mali zake. Alisema siku zote yeye hajawahi kuuona Nandy kama Tajiri au mtu mwenye pesa kama watu wengine wanavyomuona.

Billnass alifunguka kwamba kama mwanandoa yeyote baada ya harusi kukamilika anatamani kuwa na familia ila akampa Mwenyezi Mungu nafasi kubwa kwa kusema kwamba ataikubali Kamba ambavyo Muumba atakavyoiratibu.

Pindi baada ya kuweka wazi mahusiano yake na mwanamuziki Nandy, watu wengi walitoa hisia zao waking’aka kwamba mwanamuziki huyo wa muda mrefu alizama kwenye penzi la Nandy si tu kwa sababu alikuwa na mapenzi ya dhati ila kwamba alikuwana njama ya kushusha kitonga kusafiria nyota ya Nandy.

Nandy na Billnass walivishana pete za uchumba mwezi Februari mwaka huu na pia hivi majuzi wametangaza kufunga ndoa ya kifahari ambayo mwenyekiti wa kamati nzima ya kusimamia shughuli za arusi atakuwa muigizaji Steven Nyerere.

Wiki iliyopita Nyerere alitangaza kwamba harusi hiyo itakuwa kubwa mpaka kuweka wzi kwamba kamati inafikiria kuuliza ridhaa kwa mamlaka kutangaza siku ya harusi kuwa siku kuu ili kumpa kila shabiki wa wasanii hao kuhudhuria ama kwa njia ya moja kwa moja runingani au kufika mazima katika eneo la tukio hilo la kihistoria.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved