logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Huyo bibi kizee hawezi kuzalia" Mr Pimbi amchamba Harmonize kuhusu Kajala

"Sasa basi si unafaa unategemea mwanamke kabichi hivi, sasa unategemea ajuza, bibi kizee. Yule hata kumzalia hawezi" - Mr Pimbi.

image
na Radio Jambo

Habari19 July 2022 - 07:49

Muhtasari


• “Kwake inakuwa ni ngumu sana kukua kimuziki, muziki wake umeporomoka sasa hivi amebaki anategemea mwanamke" - Mr Pimbi

Muigizaji na mchekeshaji Mr Pimbi

Muigizaji mbilikimo kutoka Tanzania kwa jina Mr Pimbi amemvaa msanii Harmonize mubashara kwa kuondoka Wasafi kwa kashfa kubwa na kusema kwamba bosi huyo wa Konde Music Worldwide hawezi kamwe kumfikia kimuziki msanii Rayvanny ambaye ameondoka Wasafi wiki jana.

Akizungumza na waandishi wa habari za umbea, Mr Pimbi alisema kwamba Rayvanny ndiye msanii wa kipekee kutoka Afrika ambaye ametuzwa tuzo ya heshima kubwa ya BET na kusema kwamab licha ya mafanikio yake yote bado kijana katulia huku Harmonize bila tuzo yoyote ya maana nje ya Tanzania anatamba na kutanua kifua kweli huku akimkashfu Diamond.

Mr Pimbi alisema hata muziki wa Harmonize kwa sasa umeporomoka pakubwa na amebaki tu kumtegemea mwakamke Kajala ambaye kulingana na muigizaji huyo ni kama ajuza tu ambaye hawezi kumzalia Harmonize.

“Kwake inakuwa ni ngumu sana kukua kimuziki, muziki wake umeporomoka sasa hivi amebaki anategemea mwanamke. Sasa basi si unafaa unategemea mwanamke kabichi hivi, sasa unategemea ajuza, bibi kizee. Yule hata kumzalia hawezi, kwani ni uwongo, sayansi si ndio inasema hivo,” Mr Pimbi alifoka.

Muigizaji huyo mcheshi pia alizidi kumshambulia Harmonize huku akimpaisha Rayvanny kwa usanjari huo na kusema kwamba Vanny Boy amefanya mambo makubwa sana na msanii Macvoice ambaye alimleta kwenye gemu tayari ana mradi mkubwa sana wa ngoma na msanii kutoka Marekani, Justine Bieber.

Alisema kwamba msanii Rayvanny ni Tajiri mkubwa kupindukia sema tu ni vile hapendi kelele na miyeyusho ya mitandaoni kujionesha


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved