logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Fahamu kwa nini mwimbaji Shakira huenda akafungwa miaka minane

Mwendesha mashtaka anataka Shakira afungwe miaka 8 kwa kukukwepa kulipa kodi

image
na Radio Jambo

Habari30 July 2022 - 11:26

Muhtasari


•Mwimbaji huyo wa Colombia anashutumiwa kwa kushindwa kulipa ushuru wa €14.5m (£12m) kati ya 2012 na 2014.

Shakira anaweza kufungwa jela miaka minane na faini ya zaidi ya euro milioni 23 iwapo atapatikana na hatia katika kesi ya ulaghai wa kodi.

Mwimbaji huyo wa Colombia anashutumiwa kwa kushindwa kulipa ushuru wa €14.5m (£12m) kati ya 2012 na 2014.

Mapema wiki hii Shakira alikataa ofa ya kumaliza na kufunga kesi hiyo. Tarehe ya kesi bado haijawekwa

Taarifa kutoka kwa wawakilishi wa Shakira ilisema "ana uhakika kamili wa kutokuwa na hatia" na anaona kesi hiyo kama "ukiukaji wa haki zake".

Nyota huyo alishtakiwa kwa kukwepa kulipa ushuru mwaka wa 2018. Waendesha mashtaka walisema alikuwa akiishi Uhispania kati ya 2012 na 2014 huku akiorodhesha makazi yake rasmi mahali pengine.

Watu wanaokaa zaidi ya miezi sita nchini wanachukuliwa kuwa wakazi kulingana na kanuni ya utozaji ushuru. Lakini Shakira anasema hakuwa akiishi Uhispania wakati huo.

Hati kutoka kwa waendesha mashtaka iliyoonekana na Reuters inadai Shakira alinunua nyumba huko Barcelona mnamo 2012, ambayo ilikuja kuwa nyumba ya familia yake na mshirika wake wa wakati huo, mchezaji soka wa klabu ya Barcelona Gerard Piqué.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved