logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Staa wa Bongo Alikiba apatikana na Covid-19

Alikiba alilazimika kuahirisha  ziara yake ya muziki ya Marekani kutokana na masuala ya kiafya.

image
na Radio Jambo

Burudani02 September 2022 - 05:05

Muhtasari


•Kiba alisema  kuwa uamuzi wa kuahirisha ziara ya  'My Only One King Us Tour'  ulijiri baada ya kugundulika kuwa na maradhi ya Covid-19.

•Mwimbaji huyo amewaomba radhi mashabiki wake ambao walikuwa wameisubiri kwa hamu kwa usumbufu uliojitokeza.

Siku ya Alhamisi staa wa Bongo Ali Saleh Kiba alilazimika kuahirisha  ziara yake ya muziki ya Marekani kutokana na masuala ya kiafya.

Katika taarifa ambayo alitoa kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, Kiba alisema  kuwa uamuzi wa kuahirisha ziara ya  'My Only One King Us Tour'  ulijiri baada ya kugundulika kuwa na maradhi ya Covid-19.

"Kwa hili tunalazimika kuahirisha na kupanga upya hadi tarehe nyingine ya hivi punde kama iwezekanavyo. Hakuna kitu muhimu zaidi kwangu kuliko afya ya bendi yangu, wenzangu na ninyi mashabiki wangu," Kiba alisema.

Ziara ya 'My Only One King Us Tour' ilitazamiwa kung'oa nanga leo Ijumaa, Septemba 2  na kuendelea hadi Oktoba 1, 2022.

Kufuatia kuahirishwa kwa ziara hiyo, Kiba amewaomba radhi mashabiki wake ambao walikuwa wameisubiri kwa hamu kwa usumbufu uliojitokeza.

"Hadi wakati huo natumai kila mtu atakuwa salama na kuchukua tahadhari zote muhimu. Inshaallah tutaonana hivi karibuni," Mwimbaji huyo aliwaambia mashabiki wake.

Bosi huyo wa Kings Music Records alitazamiwa kuanza ziara yake siku ya Ijumaa katika mji mkuu wa Marekani, Washington DC.

Jumamosi alitarajiwa kutumbuiza jijini Minneapolis katika jimbo la Minnesota na baadae kufanya shoo jijini Kansas siku ya Jumapili.

Ratiba yake kwa kipindi cha ziara kilichobaki ilikuwa kama ifuatavyo:-

Septemba 10- Des Moines, Lowa

Septemba 16- Atlanta, Georgia.

Septemba 17- Lexington, Kentucky

Septemba 23- Manchester,New Hampshire

Septemba 24- Chicago, Illinois

Septemba 30- Los Angeles

Oktoba 1- Houston, Texas.

Kisa cha kwanza cha COVID-19 kiliripotiwa kwa mara ya kwanza katika  jiji la Wuhan, Uchina, tarehe 31 Desemba 2019.

Nchini Tanzania, kisa cha kwanza kiliripotiwa jijini Arusha mnamo Machi 16, 2020 kabla ya kusambaa katika maeneo mengine.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved