logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Lil Baby adhibitisha kutumbuiza mashindano ya Kombe la Dunia Qatar

Wasanii mbali mbali tayari wameanza kudhibitisha kushiriki katika kutumbuiza kwenye kipute hicho.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri23 September 2022 - 13:23

Muhtasari


• Gwiji huyo mwenye kipaji komavu ameimba albamu ya  ‘The World is Yours To Take'

Msanii huyo amedhibitisha kutumbuiza katka mashindano ya Kombe al Dunia

Mwanamuziki maarufu kutoka Marekani Lil Baby  amedhibitisha kuwa atakua miongoni mwa wasanii wa kutumbuiza katika kipute cha kombe la duni cha mwaka huu nchini Qatar.

Lil Baby alijulikana sana mwaka wa 2017, kwa kibao chake kiitwacho ‘My turn’ na ‘Harder Than Ever.’

Mwanamuziki huyo akizungumza kwenye mtandao wake wa Tweeter, alidhihirisha kujawa na furaha,unyenyekevu na shukrani sufufu kwa nafasi hiyo ya kipekee.

Lil Baby alidhibitisha kuwa atarekodi wimbo mahususi kwa ajili ya mashindano ya kombe la Dunia ambayo yatang'oa nanga Novemba 20 hadi Desemba 18 huko Qatar.

Gwiji huyo mwenye kipaji komavu ndiye nguvu kazi nyuma ya albamu maarufu ya ‘The World is Yours To Take’ , albamu ambayo itachezwa kwenye mashindano hayo. Albamu hiyo ilitoka Septemba 23.

"Kombe la Dunia la FIFA hapa tunaenda," Lil Baby alisema.

Kwa wimbo huo, rapa huyo ameungana na wanachama wa Tears for Fears - Roland Orzabal na Curt Smith.

Kombe la dunia la mwaka huu litakuwa la kipekee kwani ndiomashindano ya kwanza tangu kuasisiwa kwa kipute hicho ambacho yatafanyika pasi na uwepo wa Malkia Elizabeth II wa Uingereza aliyezikwa mapema wiki hii.

Ufaransa witajityoma ugani kwa lengo la kutetea ubiongwa huo ambao waliupata mnamo 2018 katika mashindano hayo yaliyofanyika Urusi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved