logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sina muda wa mwanamume mwingine-Akothee kwa mpenziwe

Hii ilikuwa baada ya kuachana na mpenzi wake wa zamani Nellyoaks

image
na Radio Jambo

Yanayojiri12 October 2022 - 16:36

Muhtasari


  • Alimwambia kuwa ana bahati sana kwani amempata akiwa tayari ameshamalizana na maisha yake na amefanya kila kitu katika maisha haya

Msanii mmoja aliimba kuwa mpende akupendaye na asiye kupenda achana naye, lakini kwa msanii Akothee anaonekana kukolea kwa mahaba moto moto ya mpenziwe.

Wiki chache zilizopita, mwanamuziki huyo ​​alimtambulisha mpenzi wake mpya kwa Wakenya jambo ambalo liliwaacha wengi wakimpongeza kwa mafanikio hayo mapya.

Hii ilikuwa baada ya kuachana na mpenzi wake wa zamani Nellyoaks ingawa hakushiriki sababu ya kuachana naye.

Kupitia kwenye ukurasa wake rasmi wa instaram alimwandikia na kumweleza mpenzi huyo  jinsi anavyompenda sana.

Alimwambia kuwa ana bahati sana kwani amempata akiwa tayari ameshamalizana na maisha yake na amefanya kila kitu katika maisha haya kwa uwajibikaji ambapo kukutana naye kilikuwa kitu pekee kilichobaki.

"Ni sisi tena, mpenzi unajua umenipata nikiwa nimemalizana na maisha ,nimefanya yote maishani mwangu na kwa kuwajibika sana, kitu pekee nilicho nacho. sikuwa nimefanya katika maisha yangu ilikuwa kukutana na wewe na kukupenda

Sasa tangu nilipokutana na wewe, nimekupa kila kitu, asali unachokiona ndicho unachokipata, mapenzi yangu kwako yanaongezeka kila siku,"Alisema Akothee.

Aliendelea na kumwambia kwamba hana macho wala wakati wa kuwa na mwanamume mwingine yeyote kwa sababu macho yake yana shughuli nyingi ya kumvutia.

Alimalizia kwa kusema kuwa anampenda, anamkubali, na kila wanapokuwa wawili tu huwa anafikiri anaota kwani bado haijampata kuwa yeye ni wake. Je, una maoni gani kuhusu wanandoa hao?

"Sina macho wala muda na mwanaume yeyote kwa sababu macho yangu yana kazi ya kukushangaa. I love you, admire you twin my, everytime tukiwa wawili tu mimi huwa NADHANI NINAOTA Bado haijanipata kuwa wewe ni wangu. MR OMONDI wangu nakupenda Deno."

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved