logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Betty Kyalo amtungia mama yake ujumbe maridadi siku yake ya kuzaliwa

Betty alieleza jinsi mama yake amekuwa akimuunga mkono kwa chochote anachofanya

image
na Radio Jambo

Makala27 October 2022 - 11:03

Muhtasari


• Betty alimshukuru mama yake kwa kuwa rafiki yake wa dhati na kumwelekeza kimaisha.

Mwanahabari Betty Kyalo amesherehekea siku ya kuzaliwa ya mama yake leo Alhamisi Oktoba 27.

Katika ukurasa wake wa Instagram, Kyallo alipakia picha za kumbukumbu za mama yake na yeye na kusema jinsi anavyompenda na kumthamini.

Alimshukuru mama yake kwa kumuunga mkono wakati wowote na kumwelekeza kama binti yake ingawa yeye ni mtu mzima.

"Mama mpendwa. Heri ya kuzaliwa. Wewe ni malkia wa kweli . Wewe ni mfano bora unaoeleza nguvu na neema. Wewe ni mtu mrembo na mwenye roho safi. Utaishi kuwa shujaa wangu milele," mama huyo alisema.

Betty alizungumzia uhusiano wake na mama yake ambao ni wa karibu na alivyojfunza mengi kutoka kwake.

Alieleza jinsi mama yake ni mtu bora, si kwake peke yake bali kwa kila mtu anayehusika naye.

"Unapendwa na kuthaminiwa nami. Umenifunza mambo mengi makubwa na umeushika mkono wangu katika kila hatua ya safari yangu. Wewe ni shabiki wangu mkubwa kwa chochote ninachofanya. Unanipa uwezo wa kuendelea na kunishauri kila uchao," Kyallo aliandika.

Mama huyo wa mtoto mmoja alisema kuwa anafahamu anachokitarajia sana mama yake katika maisha yake.

"Najua ombi lako kwangu na ninajua kuwa Mungu atakusikiliza! Nakupenda sana malkia wangu" Betty alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved