logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sitaleta mtoto hii dunia-Muunda maudhui Eve Mungai awajibu wakosoaji wake

Aliendelea kusema kwamba ataishi maisha yake na kufurahia kila sehemu yake.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri07 November 2022 - 14:10

Muhtasari


  • Shinikizo hilo linaonekana kumsukuma MwanaYouTube huyo na hatimaye ameamua kushughulikia mada hiyo tena
Instagram, KWA HISANI

Mtayarishaji wa maudhui nchini  Eve Mungai ametoa kauli ya uchungu kujibu shinikizo linalozidi kumtaka apate mimba.

Shinikizo hilo linaonekana kumsukuma MwanaYouTube huyo na hatimaye ameamua kushughulikia mada hiyo tena.

Katika taarifa ya ambayo alitoa kwa mashabiki wake mitandaoni, Eve Mungai alisema kwa ukali kwamba hatakubali shinikizo la mitandao ya kijamii.

Alibainisha kuwa hawezi kupata mtoto kwa sababu tu mashabiki wake walikuwa wakimshinikiza.

Aliendelea kusema kwamba ataishi maisha yake na kufurahia kila sehemu yake.

Aliteta kuwa wale wanaomshinikiza apate mtoto hawatashiriki majukumu ya kumtunza mtoto.

Kwa hivyo anaamini ni uamuzi wake na sio wa umma wakati anapaswa kupata ujauzito.

"Jambo moja kunihusu,sitaleta mtoto hii dunia juu ya shinikizo ya mitandoa ya kijamii!!nitaishi maisha yangu na kufurahia kila sekunde na kufanya kile nataka,Kama unasubiria Eve azae juu ya wambea kama watalisha mtoto wangu wewe mtangoja!" Ujumbe wa Mungai ulisomeka.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved