logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Anjella wamemshika akili ili aondoke" - Harmonize avunja uki,ya, atupa lawama WCB

Wapiga muziki tumebaki wawili tu, wanangu Cheed na Killy haikuwa riziki - Harmonize.

image
na Radio Jambo

Burudani15 November 2022 - 06:11

Muhtasari


• Alisema kuwa kwa sasa wamebaki wawili tu wanaopiga muziki ndani ya lebo yake ambao ni yeye na Ibraah.

Harmonize adhibitisha kuachana na Anjella

Kwa mara ya kwanza Harmonize amevunja kimya kuhusu kuondoka kwa wasanii watatu chini ya miezi miwili kutoka kwa rekodi lebo yake ya Konde Music Worldwide.

Japo hakuzungumza hadharani, msanii huyo alitumia weledi wake katika kutunga mashairi ya kimuziki kulizungumzia hilo ambapo  aliweka wazi kilichotokea kupelekea kuvunjwa kwa mikataba ya wasanii Cheed, Killy na mwanadada Anjella.

Kulingana na Harmonize, Cheed na Killy kuondoka haikuwa kwa ubaya bali ni pengine riziki haikuwa inawakubali wasanii hao na ndio maana wakafikia uamuzi wa kuondoka ili kutafuta chemchemi kwingine.

Alisema kuwa kwa sasa wamebaki wawili tu wanaopiga muziki ndani ya lebo yake ambao ni yeye na Ibraah huku akisema huenda Anjella alitekwa kifikira na tamaa tu na kuondoka.

“Wapiga muziki tumebaki wawili tu, wanangu Cheed na Killy haikuwa riziki. Dadangu Anjella wamemshika akili, waambie Konde Gang ni jeshi la mtu mbili,” Harmonize aliimba.

Pia alipakia vesi hiyo kwenye ukurasa wake wa Instagram ambapo watu walitoa maoni tofauti baadhi wakimkosoa kwa kuwataja watu kwenye mashairi yake na wengine kumsifia kwa ukakamavu alio nao katika kuyaingiza majina ya watu na kuiniana vizuri na vina vya kishairi.

“Tatizo mwanetu umepewa vesi badala uimbe vya maana, wewe unakomalia na kuwataja watu, muziki wa namna hiyo hauwezi kukupeleka kimataifa,” mmoja alisema.

“Wewe Tembo unajua mpaka unakera sana, sasa Asake wa Tandale ndio nani tena?” mwingine alimuuliza kwa utani.

Harmonize adhibitisha kuachana na Anjella

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved