logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DJ Mo amwandikia mwanawe ujumbe mtamu anaposherehekea siku yake ya kuzaliwa

Ladasha Wambo ni kifungua mimba wake DJ Mo na msanii wa nyibo za injili Size 8.

image
na Radio Jambo

Makala19 November 2022 - 06:33

Muhtasari


  • Kupitia kwenye ujumbe wake Mo amekumbuka jinsi mwanawe alibadilisha maishaa yake baada ya kuzaliwa miaka 7 iliyopita
Muraya-ladasha-size-8-mpasho

Mcheza Santuri maarufu DJ Mo amemnakilia kifungua mimba wake Ladasha ujumbe wa kipekee, siku hii anaposherekea siku yake ya kuzaliwaa.

Kupitia kwenye ujumbe wake Mo amekumbuka jinsi mwanawe alibadilisha maishaa yake baada ya kuzaliwa miaka 7 iliyopita.

Ladasha Wambo ni kifungua mimba wake DJ Mo na msanii wa nyibo za injili Size 8.

Mo alimwombea mwanawe ulinzi wake Mungu huku akikiri hamna kitu ambacho kitawatenganisha,na kuingilia upendo wao.

"Siku kama hii miaka 7 iliyopita nilikua baba kwa mara ya kwanza. Mtoto wa kike alizaliwa na maisha yangu yakabadilika. Wambo , Umetamani kuwa na miaka 7 na leo Mungu amefanikisha 😍🥰. @ladashabelle.wambo , Unajua jinsi ninavyokupenda , na nakuombea kwa Mungu akulinde daima , akuongoze na kukupa Fadhila . Hakuna kitakachokuja kati yetu."

Kwa upande mwingine msanii Size 8 alissema;

"Ni furaha iliyoje siku hii..... Binti yangu anatimiza miaka 7 😍❤️ happy birthday @ladashabelle.wambo.... Mungu amekuwa mwaminifu kweli mummy😍 💋❤️......."

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved