logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ni mchungaji wa kweli, miujiza yake si vipindi - DJ Mo amtetea mkewe Size-8

Nimekuwa naye na najua miujiza ni ya kweli sana. Nina furaha kwa sababu niko hapa kumuunga mkono - DJ Mo.

image
na Radio Jambo

Makala20 November 2022 - 12:20

Muhtasari


• Alisema kuwa ni kawaida watu kushuku miujiza ya watumishi wa Mungu kwani hajawahi ona miujiza ambayo inaaminiwa kuwa ya ukweli.

DJ Mo na mkewe Size 8

Kwa mara ya kwanza DJ Mo amejitokeza wazi na kumtetea mkewe Size 8 ambaye ni mchungaji na mwinjilisti.

Kwa muda sasa watu wamekuwa wa kutilia shaka maombi ya Size 8 ambapo amekuwa akionekana kuwaombea watu huku baadhi wakisema ni mitikasi ya mitandaoni na wengine wakisema kuwa maombi yake ni ya kinafiki wala si ya kweli kama anavyojiita mchungaji na mtumishi wa Mungu aliyetawazwa miaka michache iliyopita.

Akizungumza na mwanablogu Mungai Eve, DJ Mo alisema kuwa mkewe ni muombaji wa kweli na kutoa mfano kuwa maombi yake kwa mtu mmoja yalimponya kikweli na kuwa si mitikasi ya mitandaoni.

“Mimi ningekuwa nashangaa sana kama watu hawangemkejeli mke wangu. Vinginevyo, ningekuwa kama, ngoja mke wangu unafanya kitu kibaya. Ikiwa miujiza ni ya uwongo, basi ile ya kweli iko wapi? Sijawahi kuona mchungaji ambaye miujiza yake inaaminika. Nimekuwa naye na najua miujiza ni ya kweli sana. Nina furaha kwa sababu niko hapa kumuunga mkono. Nitamuunga mkono hadi mwisho,” DJ Mo alisema.

Mcheza santuri huyo wa muda mrefu aliwasuta wote wanaodhani kwamba Size 8 anatafuta kiki na neon la Mungu kuonekana akiwaombea watu na kufanya miujiza katika sehemu mbali mbali za nchi.

Alitolea mfano kwamba miezi michache iliyopita Size 8 alifanya muujiza eneo la Kibwezi alikokuwa anahubiri kwa kumuombea mtu mmoja ambaye hawakuwa wanajuana na akapona.

“Kuna madam alipona na hawajuani, alikuja hapo Kibwezi. Unajua mtu anaweza sema ilikuwa kipidni mlipanga, lakini yule hata hawakuwa wanajuana, alikuja akamuombea na ikawa hivyo, kwa hivyo wale watu ambao mnategemea kuwa hawatafanya miujiza hao ndio Mungu atatumia kufanya miujiza. Watu waache kusema ni vipindi, kuna wa ukweli na kuna si ya ukweli. Lakini wewe kama mhubiri fanya tu kile unafanya, Mungu ndiye atakulipa,” DJ Mo alisisitiza.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved