logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Zuchu, Rayvanny waiwakilisha Afrika Mashariki vyema kwenye tuzo za AFRIMMA

Tuzo hizo ziliandaliwa wikendi iliyopita katika jimbo la Dallas nchini Marekani.

image
na Radio Jambo

Makala21 November 2022 - 06:01

Muhtasari


• Zuchu alimsifia bosi wake Diamond Platnumz na kumtaja kama shujaa wake ambaye muda wote na siku zote atasalia katika kumbukumbu ya moyo wake.

Zuchu na Rayvanny washinda tuzo za Afrimma

Wikendi iliyopita wasanii Zuchu na Rayvanny walipeperusha vyema bendera ya ukanda wa Afrika Mashariki katika tuzo za AFRIMMA zilizokuwa zikifanyika Marekani jimbo la Dallas.

Zuchu alishinda tuzo yake ya Afrimma kwa mara ya kwanza kabisa ambapo alikuwa anawania katika kitengo cha Best Female East Africa.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa tuzo hizo, Zuchu aliwashukuru watu wa ukanda wa Afrika Mashariki wote waliomuaminia chini ya miaka miwili tu tangu atambulishwe rasmi kwenye Sanaa ya muziki wa Bongo Fleva na lebo ya WCB Wasafi.

Pia alimsifia bosi wake Diamond Platnumz na kumtaja kama shujaa wake ambaye muda wote na siku zote atasalia katika kumbukumbu ya moyo wake.

“Jana si yetu kupona kesho ni yetu kushinda 🏆ahsanteni sana kwa watu wangu wote wanakundi hii ni kwa wote. Mimi ni wa sasa na wa kesho,” Zuchu aliandika kwenye Instagram yake akifurahia kutuzwa.

 Kwa upande wake, Rayvanny ambaye ni mkurugenzi mkuu wa lebo ya Next Level Music alifurahia baada ya kushinda tuzo hiyo kwenye kitengo cha Best Male East Africa na kusema kwamba tuzo hiyo ni kwa wote waliomuaminia katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.

Rayvanny alisema kuwa katika maisha yake ameshinda tuzo nyingi lakini ile ya AFRIMMA ndio ilikuwa imekosekana na hivyo kuipata ni kama kumaliza mzunguko wa tuzo kwenye rafu yake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved