logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jux anyoosha maelezo kuhusu kutoka kimapenzi na Paula Kajala

Alisema watu walianza kumhusisha kimapenzi na Paula baada ya kuonekana akifanya challenge ya ngoma yake mpya.

image
na Radio Jambo

Habari21 November 2022 - 13:45

Muhtasari


• Nadhani ni kwa sababu aliwahi kupost akiimba wimbo wangu ‘Kiss’ na alikuwa anavaa collection yangu ya African boy - Jux.

Juma Jux azungumzia ishu ya kuchumbiana na Paula

Mwanamuziki wa RnB kutoka Tanzania Juma Jux ameamua kunyoosha maelezo kuhusu kile kinachodhaniwa kuwa ni uhusiano wa kimapenzi baina yake na mfanyibiashara wa nguo chipukizi, Paula Kajala ambaye ni mtoto wa mwigizaji mkongwe Kajala Masanja.

Katika mahojiano ya hivi majuzi na Wasafi Media, Jux alisema kuwa uhusiano wake na kijana huyo wa kambo wa msanii Harmonize ni wa kibiashara tu na wala hawajawahi kuvuka mipaka kuingia kimapenzi hata mara moja.

Msanii huyo aliwekwa kwenye kiti moto na kulazimika kuitetea video ambayo ilidaiwa kuwa Paula alionekana akiingia kwenye nyumba yake ila akakanusha madai hayo na kusema kuwa hata hajawahi fika katika makazi yake.

Alisisitiza kwa kumtaja Paula kama dadake mdogo tu na wala hawezi kuingiwa na suala la kumtongoza au kumuomba kuwa wapenzi, huku akisema yeye yupo kwenye uhusiano mwingine ambao unampa Amani ya akili kupita maelezo.

"Hapana, ninachoweza kusema ni kama dada yangu mdogo. Hajawahi kuja nyumbani kwangu. Sijawahi kuona hiyo klip. Ndio, kwenye klipu, inaonekana kama nyumba yangu. Sikumbuki ni muda gani nilimuona. Ukweli ni kwamba, yeye ni msichana mdogo ambaye namuona akifanya mambo yake. Hatuko kwenye uhusiano kwa sababu niko kwenye uhusiano wangu mwenyewe,” alisema.

Mdanii huyo mwenye sauti nzuri ya kusifiwa na wanawake pamoja pia na mitindo yake ya kuvaa alikisia kuwa huenda watu walianza kumhusisha kuwa kimapenzi na Paula baada ya kuonekana akifanya challenge ya wimbo wake mpya wa Kiss Ambao amewashirikisha magwiji wa Amapiano kama kina Marioo.

 “Nadhani ni kwa sababu aliwahi kupost akiimba wimbo wangu ‘Kiss’ na alikuwa anavaa collection yangu ya African boy. Sijui kwanini anahusishwa na mimi."

Rayvanny baada ya kusemekana kuwa kweney uhusiano wa kimapenzi na mwanamuziki Rayvanny, hivi karibuni mwanamuziki huyo aliweka wazi kwamab alilazimika kukatisha uhusiano wake na binti huyo wa Kajala kutokana na mambo mengi kupishana baina yao.

Kwa upande wa Jux, tangu kubwagwa na mwanamuziki na pia aliyekuwa mtangazaji Vanessa Mdee, amekuwa akiweka maisha yake ya kimapenzi nyuma ya pazia sana kiasi kwamba hakuna anayejua anachumbiana na nani.

Vanessa Mdee alitimkia Marekani na kuolewa na mwanamuziki Rotimi ambaye hivi majuzi wametangaza kutarajia mtoto wa pili pamoja.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved