logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msione nacheza Tiktok, kwa akili pia nasoma - Azziad baada ya kuhitimu

Mwanatiktoker huyo alihitimu kutoka chuo anuwai cha KIMC katika kitivo cha uanahabari.

image
na Radio Jambo

Burudani24 November 2022 - 08:57

Muhtasari


• Msinione huku mitandaoni nacheza video na huko Tiktok, pia kwa akili tunasoma,” Aziad alisema.

Nasenya ahitimu kutoka KIMC

Mwanatiktoker Azziad Nasenya ni mtu mwenye furaha baada ya kuhitimu kutoka chuo anuwai cha KIMC na shahada ya uanahabari.

Azziad alifichua habari hizo kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii na kuseam kwamba mwisho wa siku amefanikisha ndoto yake licha ya wengi kudhania kuwa hakuwa anafanay kitu cha maana mbali na kuonekana akifanya mitikasi kwenye klipu mitandaoni.

“Elimu ina njia ya kipekee ya kutufanya tuwe na muongozo mzuri wa kufikiria kwa njia sahihi na ndio maana tunafaa kuipata vizuri sababu inatutambulisha jinsi tulivyo. Msinione huku mitandaoni nacheza video na huko Tiktok, pia kwa akili tunasoma,” Aziad alisema kwenye video moja aliyoipakia kwenye instastory yake.

Mwanadada huyo alisisitiza kwamba maombi kwa Mungu ndicho kitu kilichomfanya kumudu mpaka kuhitimu katikati ya kuwa na shughuli nyingi kutoka kuwa na kazi ya redioni asubuhi.

Alisema masomo yake ilimbidi kuyafanya wakati wa ziada jioni baada ya kumaliza kufanya shughuli zingine za siku na aliendelea na mzungumzo huo mpaka kumaliza na kuhitimu.

“Kama si Mungu na kujitolea, kujitutumua usiku na mchana, nisingekuwa hapa. Nilikuwa naamka saa 4 asubuhi kila siku. Ilikuwa ni mapambano,” Nasenya alisema.

Mwanadada huyo alijizolea umaarufu mwaka 2020 wakati wa janga la Korona  baada ya kushiriki katika kufanya challenge ya ngoma ya rapa Femi One akimshirikisha Mejja, Utawezana.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved