logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Wanaume wanalia kwa sababu ya mapenzi,'Loise Kim awashauri wanawake kuwaelewa wanaume

Kulingana naye, alisema kuwa wanaume pia wanaweza kuwa  hawana uwezo wa kifedha

image
na Radio Jambo

Burudani29 November 2022 - 09:22

Muhtasari


  • Aliendelea na kusema kwamba wanaume pia wana mahitaji ya kihisia, matatizo na bado wanalilia mapenzi na kwa hivyo wanapaswa pia kuzingatiwa

Msanii maarufu wa nyimbo za injili a kikuyu Loise Kim kupitia kwenye ukurasa wake wa Facebook amewashauri wanawake kuwaelewa wanaume wakati mwingine kwani wao pia ni binadamu.

Kulingana naye, alisema kuwa wanaume pia wanaweza kuwa  hawana uwezo wa kifedha na kujifanya kuwa kila kiko sawa kwani wakati mwingine hawana kila kitu ambacho mwanamke anahitaji kutoka kwao.

Aliendelea na kusema kwamba wanaume pia wana mahitaji ya kihisia, matatizo na bado wanalilia mapenzi na kwa hivyo wanapaswa pia kuzingatiwa.

"Wanaume wanaweza kushindwa kifedha na kujifanya wana kila kitu. Wakati mwingine, hana vitu unavyotaka. Wana mahitaji na matatizo ya kihisia. Wanaume bado wanalia kwa ajili ya upendo,"Loise Kim alisema.

Wakenya walikuwa kote katika sehemu ya maoni wakikubaliana naye wakisema alikuwa sahihi kwamba wanaume pia ni binadamu.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved