logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Uchungu moyoni ni ule ule,'Sandra Dacha awaomboleza wazazi wake

"Wakati fulani natamani ungekuwa hapa ili niweze kukuambia ni kiasi gani ninakuhitaji ...

image
na Radio Jambo

Yanayojiri30 November 2022 - 08:40

Muhtasari


  • Mwigizaji huyo alitamani kutumia tu saa moja na wazazi wake.Sandra alifahamika kupitia uigizaji wake kwenye kipindi cha Auntie Boss
Sandra Dacha

Mwigizaji Silprosa almaarufu Sandra Dacha amewaacha mashabiki na wanamitandao wakimtumia jumbe za pole baada ya kuwaomboleza wazazi wake.

Katika ukurasa wake wa facebook, alichapisha picha akiwa amesimama kando ya makaburi ya wazazi wake na kuandika maandishi marefu yenye kugusa moyo.

Katika ujumbe huo aliandika jinsi anawakosa wazazi wake, licha ya kutabasamu kila siku.

Mwigizaji huyo alitamani kutumia tu saa moja na wazazi wake.Sandra alifahamika kupitia uigizaji wake kwenye kipindi cha Auntie Boss.

Alisema,

"Wakati fulani natamani ungekuwa hapa ili niweze kukuambia ni kiasi gani ninakuhitaji ... naficha machozi yangu ninapotaja jina lako lakini UCHUNGU moyoni mwangu bado ni ule ule... ingawa ninatabasamu na kuonekana bila kujali lakini hakuna anawakukosa kama mimi.Je, ninachagua kuamka kila siku na kuhuzunika?HAPANA!Ninaamka kila siku na najua sehemu yangu haipo.

Ikiwa ningeweza kutoa matakwa moja na nisiwe na lingine, ingekuwa kuwa na saa moja na kuitumia pamoja nawe,"Aliandika Sandra.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved