logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Bila wewe Yamoto Band haingefaulu - Beka Flavour amsifia Aslay

Bila wewe sisi wengine tungechelewa kufaulu - Beka Flavour alimwambia Aslay.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri01 December 2022 - 05:19

Muhtasari


• Karibu tena kwenye uwanja wako Mkang’afu mashabiki zako tulikukosa sana na umerudi kwa kishindo na ngoma mbili - Beka Flavour.

Beka Flavour amsifia Aslay

Beka Flavour, msanii ambaye alikuwa mmoja wa bendi ya Yamoto na wenzake Aslay, Enock Bella na Mbosso amefurahia urejeo wa Aslay kwenye kuandika na kutunga tena mashairi ya muziki  baada ya kimya cha muda mrefu.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Beka Flavour amemkaribisha Aslay, rafiki wake wa muda mrefu na kumtamkia maneno ya kheri.

Alsay baada ya kusainiwa na lebo za RockStar na Sony Music Entertainment, aliingia studioni na kuachia ngoma mbili, ya kwanza ikiwa kama kumbukumbu ya mama yake Mozzah huku ya pili ikiwa ni collabo aliyomshirikisha kamanda wa shughuli hizo, Harmonize kwa jina Follow Me.

Hizi ngoma zinakuja wiki moja tu baada ya kuachia mfululizo wa filamu hadi vipindi 5 akizungumzia maisha yake kwa jumla tangu alipoanza muziki hadi kufikia hapo alipo sasa.

Beka Flavour alimsifia na kumwambia kwamba yeye ndiye alileta ufanisi katika kundi la Yamoto na bila yeye wengine hawangemudu kufanya muziki wa biashara mpaka sasa.

Karibu tena @aslayisihaka mimi nakuita fundi wa huu mziki ndugu yangu hatujazaliwa pamoja lakini moyo wako ni wa kipekee sana, binafsi naamini bila wewe kukunjua nafsi yako na kukubali kutubeba sisi ndugu zako kwenye wimbo wetu wa kwanza uliotutambulisha kama bendi lakini kama wasanii wapya kwenye gemu hili inawezekana tungetoka lakini kwa kuchelewa kidogo, karibu tena kwenye uwanja wako Mkang’afu mashabiki zako tulikukosa sana na umerudi kwa kishindo na ngoma mbili,” Beka aliandika.

Aslay, baada ya kusambaratika kwa kundi la Yamoto, alianza kufanya kazi kama msanii wa kujitegemea ambapo alifana sana ila hapa kati akaja kupotea kabisa kiasi kwamba mashaiki zake hawakuwahi kumsikia kwa zaidi ya mwaka mzima.

Katika filamu hiyo ya Mimi ni Bongo Fleva, msanii huyo alipata kuzungumzia mengi yaliyokuwa yakiendelea nyuma ya pazia katika maisha yake huku akisema kuwa aliumia sana kumpoteza mama yake lakini pia kusongwa na mawazo, ulevi na wanawake karibia vimsafirishe jongomeo kabla siku yake kuwadia.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved