logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanaume kama mpenzi wako hamjui Rio Ferdinand, huyo hakufai - Larry Madowo ashauri

adowo alikutana na Ferdinand nchini Qatar kabla ya mechi ya Ufaransa na Morocco.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri15 December 2022 - 09:47

Muhtasari


• Madowo ni mwanahabari wa runinga ya kimataifa ya CNN na alikuwa nchini Qatar kufuatilia mechi ya nusu fainali.

Larry Madowo na Rio Ferdinand

Mwanahabari wa kituo cha kimataifa cha runinga CNN, Larry Madowo ni mu mweney furaha baada ya kukutana na aliyekuwa beki matata wa timu ya Manchester United, Rio Ferdinand katika moja ya viwanja vinavyotumiwa kuandaa mashindano ya kombe la dunia huko Qatar.

Madowo alifurahia wakati mzuri na mchezaji huyo wa zamani na hakusita kupasua mbarika kwa habari hizo kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii ambapo alisema kukutana na mtu ambaye alikuwa anamtizama kwenye runinga ni kama kufanikisha ndoto yake.

Pia aliwashauri wanaume kuwa kama mpenzi wako wa kike hajui Rio Ferdinand ni nani basi wewe kama mwanaume jua huyo ni mdogo sana na hafai kuwa mpenzi wako.

“Nilikutana na Rio Ferdinand kabla ya mechi ya Ufaransa Morocco. Ikiwa hajui Rio ni nani, yeye ni mdogo sana kwako kaka!” Madowo alisema.

Wafuasi wake na ambao walikuwa mashabiki sugu wa kandanda na premia Uingereza EPL walimtaja Ferdinand kwa kumbukumbu mbalimbali huku wakimtaka Madowo kutuma salamu zake.

“Hii inanikumbusha wakati Manchester ilipokuwa Manchester United...uyu ni bazenga..Rio Ferdinand ni mtu mwenye bahati sana,” Mbaya Ken aliandika.

“Lwejendari wa Man U tunamfahamu sana, nisaidie kumuuliza anakumbuka Gareth Balamy na man city ni nani?” Collins Anderson aliuliza.

Wengine walichambua kauli yake na kusema kuwa ikiwa watapata wapenzi wasiomjua Ferdinand, huenda watawasamehe lakini katu hawawezi kusamehe iwapo hawatakuwa wanamjua Messi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved