logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ushauri wa Anerlisa kwa wanawake wanaowachumbia wanaume walio kwenye ndoa

Aidha wanaume wenyewe hawajalaza damu kwani wamekuwa wakikimbizana na wasichana hao

image
na Radio Jambo

Makala15 December 2022 - 17:16

Muhtasari


  • Mwanabiashara maarufu Anerlisa Mungai kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram amewashauri wasichana hao

Je kama mwanamke umewahi furahia kumchumbia mwanamume ambaye anafamilia yaani mke na watoto?

Ni mtindo ambao wasichana wachanga kutoka chuo kikuu wamejizoesha kwa kuwachumbia wanaumee ambayo tayari wwana familia.

Aidha wanaume wenyewe hawajalaza damu kwani wamekuwa wakikimbizana na wasichana hao, huku wakidai kwamba wana damu joto.

Mwanabiashara maarufu Anerlisa Mungai kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram amewashauri wasichana hao.

"Wakati wa ukimya kwa wale wanawake wanaokuja kwenye uhusiano wakidhani watakuwa bora kuliko mke

Shida ni kwamba unaona wanaume wanapendeza kwenye mitandao ya kijamii, bila kujua kuwa mke ndiye aliyemuweka pamoja kwa hiyo ukipewa nafasi hiyo huwezi kuendelea na hilo."

Je unaweza tamani kuwa na mwanamke mwingine bali na mke wako, au kama wewe ni mke unaweza fanya aje ukimpata mwanamume wako na mwanamke mwingine, na bali sio wa umri wwako lakini ana umri wa chini.

Wengi wamejipata katika hali hiyo na kisha kuwaacha waume zao, kwani huwa wanahisi kusalitiwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved