logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Chifu aliyerekodiwa akidensi klabuni adai alikuwa akichunguza matumizi ya dawa za kulevya

Migun alisema alikuwa ameenda kufanya kazi ya siri.

image
na

Habari10 January 2023 - 10:20

Muhtasari


•Chifu Msaidizi ambaye video yake akicheza densi kwa ustadi katika kilabu ilivuma kwenye mitandao ya kijamii, amesema alikuwa ameenda kufanya kazi ya siri.

•"Nilipokuwa nikicheza, mtu niliyekuwa naye alinirekodi na sikutarajia kwamba ingeenea mtandaoni." Alisema.

, Chifu Msaidizi wa eneo moja katika Kaunti ya Kisumu amesema alikuwa kwenye kazi ya siri katika klabu.

John Ogilo Migun, Chifu Msaidizi wa eneo moja katika Kaunti ya Kisumu ambaye video yake akicheza densi kwa ustadi katika kilabu ilivuma kwenye mitandao ya kijamii, amesema alikuwa ameenda kufanya kazi ya siri.

Katika mahojiano na Citizen Digital, Migun alisema alikuwa ameenda kwenye klabu hiyo kuchunguza janga la utumizi wa dawa za kulevya.

"Baada ya kazi, tulikua tumeenda mambo ya undercover kuhusu matumizi ya dawa za kulevya, ghafla wimbo ambao napenda ukachezwa, nafahamu huo mziki na naupenda," alisema.

Migun alisema alipokuwa akinengua kiuno, kijana aliyekuwa naye alianza kumrekodi na hakujua kuwa video hiyo ingesambaa mitandaoni.

"Nilipokuwa nikicheza, mtu niliyekuwa naye alinirekodi na sikutarajia kwamba ingeenea mtandaoni." Alisema.

Aidha alieleza kuwa video hiyo imemsaidia kutangamana na vijana, hivyo kuwapa uhuru wa kufunguka kwake kuhusiana na masuala yanayowahusu.

“Tangu video hiyo kusambaa, nimekuwa nikitangamana na vijana kwa uhuru, wanakuja ofisini kwangu bila woga kunieleza masuala yao,” alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved