logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nilikuwa milionea nilipokuwa miaka 17-KRG the Don ajigamba

Alisema kwa sasa yeye ni tajiri kuliko wasanii wote wa Kenya kwa pamoja.

image
na Radio Jambo

Makala10 January 2023 - 11:11

Muhtasari


  • Alisema kwa sasa yeye ni tajiri kuliko wasanii wote wa Kenya kwa pamoja
  • Alisema kuwa itamchukua mwanamuziki wote wa Kenya, miaka 10 ya kufanya kazi kwa bidii ili kuwa tajiri katika kiwango chake cha utajiri
Instagram, KWA HISANI

Mmoja wa wanamuziki tajiri maarufu wa dancehall nchini Kenya, Krg the Don amesema kwamba alikuwa milionea alipokuwa na miaka 17 kwa sababu alikuwa na busara sana, na aliwekeza vizuri sana pesa ndogo alizopata.

Akizungumza katika mahojiano na Mungai Eve, Krg ameendelea kusisitiza kuwa yeye ndiye msanii tajiri zaidi nchini Kenya.

Krg alisema kuwa anaunda urithi utakaomfanya akumbukwe na Wakenya kwa miaka 650 ijayo.

Alisema kwa sasa yeye ni tajiri kuliko wasanii wote wa Kenya kwa pamoja.

Alisema kuwa itamchukua mwanamuziki wote wa Kenya, miaka 10 ya kufanya kazi kwa bidii ili kuwa tajiri katika kiwango chake cha utajiri.

Kulingana na Krg, pesa ndio kila kitu na huwa anafikiria jinsi atakavyoongeza faida yake na ndio maana huwa anatembea na matajiri.

Krg alisema kuwa anatoza Ksh.1 Milioni kwa kutumbuiza katika onyesho lolote la Arena.

Kwa uchezaji wa vilabu anatoza ksh.500000 , kwa kila uchezaji na hiyo ndiyo sababu yeye hucheza mara chache katika vilabu, kwa sababu vilabu vingi haviwezi kumudu.

Aliendelea na kusema kwamba anatoza ksh.250,000 , kwa kufuata watu kwenye Instagram.

Sababu kubwa ya kufanya hivyo ni kwa sababu, yeye ni brand na pia ni mshauri kwa wengi.

Krg alisema kuwa yeye hategemei muziki, anafanya kwa burudani tu. Alisema kuwa yeye ni mfanyabiashara aliyefanikiwa sana na ni miongoni mwa mabilionea watano bora nchini Kenya.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved