logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Chege Chigunda atangaza kuoa miezi 3 baada ya video ya uchi wake kuvujishwa

Alisema anachokihitaji kutoka kwa mwanamke ni heshima, upendo na usikivu.

image
na Radio Jambo

Habari13 January 2023 - 09:48

Muhtasari


• Chege ni mwanamuziki wa muda mrefu ambaye alitamba na kundi la TMK Wanaume Family.

Chege kuoa mwaka huu

Msanii wa muda mrefu wa Bongo Fleva Chege Chigunda ametanaza kuwa mwaka huu wa 2023 Inshalllah atafunga ndoa.

Chege aidha alidokeza kuwa japo anatarajia ndoa lakini bado hajapata mwanadada wa kufunga ndoa naye, kwani ndoa si ya mtu mmoja bali ni wawili – mke na mume.

Aliwataka wanawake wote ambao wanajiona au kujihisi kuwa wana nafasi ya kuwa mke halali kwake kujiongeza huku akisema wanaume wanahitaji mambo machache sana kutoka kwa wanawake.

Akijitolea mfano, Chege alisema kuwa vitu anavyovitegemea kutoka kwa mwanamke wa kumuoa ni heshima, mapenzi na usikivu tu basi.

“Wanadada jiongezeni wanaume tunahitaji mambo machache sana,mfano mie Ukinipenda, Ukiniheshimu, Ukiniskiliza tu basi. Naoa mwaka huu huu 2023 chap,” Chege aliandika.

Tangazo hili linakuja mieizi mitatu tu tangu Staa huyo aliyetamba na kundi la wanamuziki la TMK kuanikwa hadharani kwenye mitandao ya kijamii baada ya video yake chafu alionekana kupiga punyeto akijirekodi huku akipapasa uume wake kuvujishwa na yule aliyesemekana kuwa mwanadada ambaye alitumiwa klipu ile.

Sekeseke hizo za mitandaoni zilisambaa kwa kasi kama moto wa jangwani huku msanii huyo akiwa amefyata ulimi na kufunga mdomo wake kwa muda huo wote wakati ambapo mashabiki wake walikuwa wanasubiria kusikia atajitetea akiwa upande gani kuhusiana na ile klipu ambayo inamuonesha kabisa mpaka uso wake pamoja na utupu wake wa mbele.

Kama wewe ni mwanadada na uliona klipu ile, maamuzi ni yako kama kujaribu bahati au kulenga tu!

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved