Wacheni kuwashambulia side chicks wakati tatizo ni waume wenu-Mwigizaji Nyaboke

Miaka miwili iliyopita, Mwigizaji Gloria Moraa almaarufu Nyaboke alifichua jinsi alivyotoroka na kwenda kuolewa

Muhtasari
  • Nyaboke alisema kuwa Side Chicks hawana hatia kwani wanalishwa uongo na wanaume waliooa hivyo kuangukia kwenye mitego yao
Muigizaji Nyaboke ajisherehekea kufikisha miaka 38
Muigizaji Nyaboke ajisherehekea kufikisha miaka 38
Image: Instagram

Wacheni kuwashambulia Side Chicks wakati tatizo ni waume wenu haya ni matamshi ya mwigizaji Nyaboke Moraa huku akiwashauri wanawake walioolewa.

Nyaboke alisema kuwa Side Chicks hawana hatia kwani wanalishwa uongo na wanaume waliooa hivyo kuangukia kwenye mitego yao.

"Hiyo gaidi yako ilimwambia ulikufa, ama mlidivorce ama mnaishi vyumba tofauti. Hiyo gaidi zimezoea na bibi anazaa kila mwaka.Hivyo ukijua mumeo ana side chick nenda kamshambulie. Acha kuwashambulia wasichana wasio na hatia ambao wameambiwa mambo mengi ya kipuuzi,” aliongeza.

Miaka miwili iliyopita, Mwigizaji Gloria Moraa almaarufu Nyaboke alifichua jinsi alivyotoroka na kwenda kuolewa mara baada ya kumaliza shule ya upili.

Mashabiki walichangia ujumbe wake na haya hapa maoni yao;

queenobayi: 🤣🤣🤣🤣vile inafaaa, ama watembe na Gaidi zao kwa mfuko, Uuupuuuuus!

richard_yu_alfred: ambassador wewe ujui boychild ako delicate 😂😂🙌🇰🇪

mercy_jjoseph: Ongezako volume please.Ati ooh,mbona unachukua bwana yangu?kwani ni cabbage?!

m_jackie_b: Very true wanasema bibi alikufa juu ya cancer na kumbe bibi ako much alive

njagisr_victor: Utafanya wanawake wauliwe wakienda kupiga bwana zao,watu watulie ama warudi soko😂😂😂