logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Ninarejea shuleni" Trio Mio afichua kozi anayotaka kusomea katika Chuo Kikuu

Trio alifichua kuwa atafanya kozi ya Ubunifu wa Picha na utayarishaji wa muziki.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri22 January 2023 - 05:45

Muhtasari


•Trio alifichua kuwa atafanya kozi ya Ubunifu wa Picha na utayarishaji wa muziki (Graphic Design & Music Production).

•Trio Mio alikataa kuweka wazi hadharani matokeo yake ya KCSE, akisema atafanya hivyo kwa wakati ufaao.

Mwanamuziki wa nyimbo za kufoka Trio Mio amefichua kozi anayotaka kusomea katika chuo kikuu baada ya kutolewa kwa matokeo ya mtihani wa KCSE 2022.

Akiwa kwenye mahojiano na Jalang’o kwenye kipindi cha Bonga na Jalas, Trio alifichua kuwa atafanya kozi ya Ubunifu wa Picha na utayarishaji wa muziki (Graphic Design & Music Production).

"Kwa sasa ninarejea shuleni na nitajitosa katika utayarishaji wa muziki wa Ubunifu wa Picha ambayo tayari ni kazi yangu - kitu ambacho napenda kufanya na kinaniingizia pesa.

Utayarishaji wa muziki uko hivyo na watu kama Boutrosss wananitia moyo sana," Trio Mio alisema.

Hata hivyo, mwimbaji huyo wa kibao ‘Achia’ alikataa kuweka wazi hadharani matokeo yake ya KCSE, akisema atafanya hivyo kwa wakati ufaao.

"Wakati ukifika nitawaambia lakini sasa hivi tuzingatie muziki…," Mio aliongeza.

Wakati wa mahojiano, rapa huyo pia alizungumzia unyanyasaji wa mitandaoni dhidi yake - akifichua memes na matusi ambayo yalimgusa zaidi.

“Kuna mtu alisema muziki wangu unavuma zaidi ya muziki wake… na wengine walisema nimepata D.

Ilinifanya nifikirie ikiwa ninafaa kuboresha muziki wangu au nini lakini wakati huohuo ilinipa changamoto ya kufanya vyema zaidi,” Trio Mio alieleza.

Trio pia alitaja idadi nzuri ya majina ya mastaa ambao wanamtia moyo; Khaligraph Jones, Nadia Mukami, na Savara huku collabo yake ya ndoto yake ya kimataifa akiwa ni na Zinoleesky wa Nigeria.

Ufichuzi wa Trio Mio kuhusu taaluma atakayofuata unakuja baada ya kutolewa kwa matokeo ya KCSE 2022 na Waziri wa Elimu Ezekiel Machogu siku ya Ijumaa.

Baada ya kupokea matokeo yake, Trio Mio aliwapongeza watahiniwa wenzake wote ambao walipata matokeo yao pia.

Akizungumza kupitia ukurasa wake wa Instagram, msanii huyo mwenye umri wa miaka 18 aliwatia moyo waliokuwa watahiniwa wenzake na kuwahakikishia kuwa wote walijitahidi kadiri ya uwezo wao.

"Hongera kwa watahiniwa wote ambao wanapokea matokeo yao leo. Sote tulijitahidi kufikia hatua hii muhimu. Ndio maisha yanaanza na nawatakia bahati kwa yote ambayo mnapanga kufanya 💯❤️," aliandika


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved