logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Anahitaji huruma- Karen Nyamu amjibu Samidoh baada ya kumwita chura

"Huyo ni msichana wangu, unakaa mrembo wakitutukana chura tunaruka ruka mbele

image
na Radio Jambo

Yanayojiri25 January 2023 - 16:45

Muhtasari


  • Kupitia kwenye ukurasa wa facebook wa Karen alichapisha ujumbe ambapo alisema kwamba hakuwa peke yake tangu wakati wote na kila msimu Mungu alitembea pamoja naye
Nyamu asema haachi pombe

Siku chache zilizopita Samidoh na Karen Nyamu walishambuliana mitandaoni  na kuwaacha wanamitandao na hisia mseto.

Baada ya Karen kuanzisha pambano hilo na kumwita Samidoh kuwa ni mtu ambaye hajatahiriwa, Samidoh alishindwa kuzuia hasira ambapo aliamua kumrushia Nyamu cheche za maneno.

Samidoh alisema kuwa hata iweje hawezi kupeleka chura kwa mama yake ili kuwafurahisha watu ambapo alikuwa akimtaja Karen Nyamu kama mjeledi.

Kupitia kwenye ukurasa wa facebook wa Karen alichapisha ujumbe ambapo alisema kwamba hakuwa peke yake tangu wakati wote na kila msimu Mungu alitembea pamoja naye.

Mmoja wa wafuasi wake alitoa maoni akisema kuwa anaonekana mrembo hata kama mtu angemwita chura.

"Huyo ni msichana wangu, unakaa mrembo wakitutukana chura tunaruka ruka mbele,"Aliandika shabiki.

Karen alijibu hili akisema mwanamume anapofikia hatua hiyo ya kumtusi mwanamke anahitaji huruma na watu wasimhukumu.

Aliendelea na kusema kama angejua kuwa chura hamhitaji tena angekuwa tayari amefuta maoni hayo.

"Mwanaume akifika hio point anahitaji huruma dont judge him. Kwanza akikumbuka hio chura ata haina kazi yake inabidi adelete tu hio comment😂😂,"Aliandika Karen.

Wawili hao waliachana mwaka jana baada ya kusababisha drama Dubai.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved