logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Awinja Nyamwalo 'Jacky Vike' afurahia kupata kazi ya ubalozi serikalini

Vike alizinduliwa rasmi kama balozi Januari 30, siku ya kuadhimishwa kwa NTD.

image
na Radio Jambo

Makala31 January 2023 - 08:16

Muhtasari


• Ilikuwa ni heshima kubwa kupata jukumu hili siku ile ile tunapoadhimisha siku ya dunia kwa NTDs. Tuanze kazi Sasa - Awinja alisema.

Mwigizaji Awinja akizinduliwa kama balozi wa wizara ya afya

Mchekeshaji Awinja Nyamwalo almaarufu Jacky Vike ni mtu mwenye furaha baada ya kupata kazi ya ubalozi katika serikali ya Kenya Kwanza ikiongozwa na rais William Ruto.

Awinja alipakia video kwenye mitandao yake ya kijamii na kufichua kwamba hatimaye ametambuliwa kama balozi wa kutoa hamasisho kwa jamii kuhusu madhara ya Magonjwa ya Kitropiki Yaliyopuuzwa.

Awinja alionesha furaha hiyo na kusema kuwa imekuwa ni ndoto yake siku moja kufanya kazi na wizara ya Afya nchini ili kutoa tahadhari kuhusu magonjwa mbali mbali ambayo yanawasumbua watu na yanaweza kuzuiliwa kwa njia nyepesi tu.

“Mabibi na Mabwana nawapa Balozi mpya wa Magonjwa ya Kitropiki Yaliyosahaulika (NTDs) Ilikuwa ni heshima kubwa kupata jukumu hili siku ile ile tunapoadhimisha siku ya dunia kwa NTDs. Tuanze kazi Sasa😁. Asante Wizara ya Afya - KENYA AIHD Kenya kwa fursa ya kuhudumia jamii,” Awinja aliandika.

Awinja alizinduliwa rasmi Januari 30, siku ambayo duniani kote watu wanaadhimisha siku hiyo ya kutoa hamasisho kuhusu magonjwa ya kitropiki ambayo yalisahaulika kwamba yamekwisha lakini ndio yanaendelea kuwasumbua watu kinyemela.

Kupitia Instagram yake, Awinja alishiriki video fupi inayoonyesha jinsi alivyosherehekea hafla ya Siku ya NTD Duniani iliyoandaliwa katika hoteli ya Acacia Premier mjini Kisumu.

Mwigizaji huyo wa zamani wa kipidni cha Papa Shirandula aliandamana na baadhi ya waigizaji wenza katika kipindi hicho kwenda Kisumu ambapo walitoa hamasisho kuhusu magonjwa ya NTD.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved