logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nitawaambia kilichonitoa katika kuimba nyimbo za injili - Willy Paul

Alikuwa anajibu maneno ya Eric Omondi kuwa hawezi fnikiwa sababu ya kuacha injili.

image
na Radio Jambo

Makala06 February 2023 - 08:04

Muhtasari


• Eric Omondi alisema wasanii wa injili wana skendo nyingi za kuwachafua kuliko zile ambazo zinawaandama wasanii wa sekula.

Pozee aahidi kusema kilichomtoa kwenye injili

Msanii Willy Paul ameonekana kujibu tamko la Eric Omondi kuwa alitoroka kuimba miziki ya Injili na kuzamia ya kidunia.

Katika video ambayo Eric Omondi alifanya na kuipakia kwenye Instagram yake, aliuliza uwepo wa wasanii wa Injili ambao walikuwa wanatunga nyimbo nzuri za kumtukuza Mungu, ambazo mcheshi huyo alisema ndizo zilikuwa kama nembo ya kulitambulisha taifa la Kenya.

Alisema kuwa wote walizama kusikojulikana huku pia akiibua madai ya ukakasi kwamba baadhi yao wanajihusisha na vitendo vya kuvunja amri ya saba katika mtaa wa Umoja jijini Nairobi.

“Yuko wapi Bahati, yuko wapi Willy Paul…. Nakumbuka enzi za tuzo za Groove ambazo zilikuwa kubwa Zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki na kati, halafu kitu cha mwisho nilisikia ni kwamba baadhi wanafanya mapenzi katika mtaa wa Umoja, Willy Paul aliacha injili na sasa wako na skendo nyingi kuliko wasanii wa sekula…” Omondi alisema.

Aliwaambia kwamba kwa vile wamemuacha Mungu, hawatoweza kufanikiwa katika maisha yao kamwe.

Tamko hili lilijibiwa na Willy Paul ambaye alisema atatoa ufafanuzi wa kina kuhusu kilichomuondoa katika Sanaa ya injili huku akisisitiza kwamba uhusiano wake na Mungu bado haujabadilika kama ambavyo Omondi alikwa anasema.

“Nitawaambieni kilichonitoa katika Sanaa ya injili lakini pia uhusiano wangu na Mungu uko pale pale haujabadilika,” Willy Paul aliandika kwenye Instastory yake.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved