Adidas kupoteza bilioni 163 kwenye mauzo baada ya kuvunja mkataba na Kanye West

Adidas walikuwa wamefanya kazi na Kanye West kwa miaka 9 wakimsambazia nguo na viatu vya kampuni yake ya Yeezy.

Muhtasari

• Kampuni ya Adidas sasa imesema mwaka huu utakuwa mgumu kwao sokoni kwani mauzo yao yatadorora pakubwa.

Adidas yaonya kupoteza faida baada ya kuachana na Kanye West
Adidas yaonya kupoteza faida baada ya kuachana na Kanye West
Image: BBC NEWS

Kampuni ya nguo na vifaa vya michezo ya Adidas imeonya kwamba mapato yao yamepata pigo kubwa miezi 5 tu baada ya kuvunja mkataba wao na msanii rapa Kanye West mwezi Oktoba mwaka jana kufuatia matamshi yake yanayolenga kuwabagua Wayahudi – Antisemitic.

Katika taarifa zilizochapishwa kwenye vyombo vya kimataifa, Adidas walisema kuwa baada ya kukatisha mkataba wao na Ye, huenda mwaka huu wakapoteza kiasi cha takribani dola bilioni 1.3 za Kimarekani sawa na bilioni 163 za Kenya.

Adidas walivunja mkataba na Ye baada ya kufanya kazi naye kwa miaka 9 ambapo walikuwa kama mawakala wa kuuza na kusambaza nguo za chapa yake ya Yeezy.

Katika taarifa, Adidas ilisema mwongozo wake wa kifedha wa 2023 "unachangia athari mbaya kutokana na kutouza hisa zilizopo." Ikiwa kampuni haiwezi "kuuzaa tena" nguo yoyote ya Ye iliyobaki, Adidas ilisema hiyo inaweza kugharimu kampuni hiyo $534 milioni (euro milioni 500) katika faida ya uendeshaji mwaka huu.

Kampuni hiyo ilisema muda mfupi baada ya ushirikiano huo kuvunjwa kuwa ilijaribu kuuza nguo hizo, ikiwa imeondolewa jina la Yeezy na chapa. Adidas ilisema kuuza bidhaa hizo chini ya chapa yake kutaokoa kampuni takriban dola milioni 300 katika malipo ya mrabaha na ada za uuzaji.

Katika muda mwingi wa mwaka jana, Ye aliingia kwenye ugomvi na baadhi ya makundi ya watu kufuatia matamshi yake ambayo alionekana kwenda kinyume na kile ambacho wengi walikuwa wanaamini kuwa hakifai kutokea au kinafaa kutokea.

Kwa mfano, licha ya kuwa Mmarekani mweusi, Kanye West alitetea afisa wa polisi aliyemuua Mmarekani mweusi George Floyd akisema kuwa halikuwa suala kubwa, licha ya watu wengi kutoka jamii za Weusi na Weupe kuamini kwamba kitendo cha polisi yule kilikuwa cha kinyama.