logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Guardian Angel ataka Wakenya kumtumia 'sadaka' kwa kufanya ombi la mvua kwa Mungu

"Haya sasa ndio yanaitwa maombi ya ukweli, unapiga ombi, Mungu anajibu." - Angel.

image
na Radio Jambo

Makala16 March 2023 - 10:14

Muhtasari


• “Hili ndio ombi langu, kwa ajili ya nchi yangu, jua linawaka sana, mito inakauka Bwana….” Kionjo cha wimbo.

• Guardian Angel alikuwa kweney mtaa wa barabara moja katikati mwa jiji akinyeshewa wakati akirekodi video hiyo.

Guardian Angel awatanai Wakenya kumpa sadaka kwa ombi la mvua

Mwenyekiti wa miziki ya injili Kenya wa kujitangaza mwenyewe Guardian Angel amewataka Wakenya kutoa dhabiu ya sadaka kwa kile alisema kwamba Mungu hatimaye amejibu maombi ya kuleta mvua.

Alhamisi asubuhi, sehemu nyingi za Kenya, haswa Nairobi, wakaazi waliamka na Baraka mfululizo za mvua nyingi ambazo zilianza kunyesha usiku wa Jumatano.

Angel alipakia video kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa na msanii mwingine wa miziki ya kidunia Dufla Diligon ambapo alitamba kwamba ni yeye alipiga mzuka wa kibao cha maombi kwa Mungu kwa ajili ya mvua – maombi ambayo yamejibiwa hatimaye.

Msanii huyo alikuwa kwenye mtaa mmoja wa barabara za katikati mwa jiji la Nairobi akiwa ananyeshewa na manyunyu ya mvua hizo.

“Toeni Sadaka Mungu amejibu maombi. Ni kama Mungu amekubali, ametukumbuka. Unaoan niliwapigia mzuka Fulani hapo wa maombi ya ajabu, sasa mvua ndio hizi. Haya sasa ndio yanaitwa maombi ya ukweli, unapiga ombi, Mungu anajibu. Si kupandisha watu mlima bure. Huu wimbo niliutoa wiki jana na Mungu amejibu, hebu wekeni hapo sadaka…” Guardian Angel alimaliza huku akitaja namba yake ya simu kwa utani.

Msanii huyo pia aliweka kionjo cha wimbo wake wa ‘Ombi Langu’, ambao alidai kuutoa wiki jana.

“Hili ndio ombi langu, kwa ajili ya nchi yangu, jua linawaka sana, mito inakauka Bwana….” Kionjo cha wimbo huo kilisikika kikiimba kwa umbali.

Mwezi jana, rais William Ruto kwa kushirikiana na watu mbali mbali wakiwemo wakenya na wasanii walikongamana katika uwanja wa michezo wa Nyayo katika kile walisema kuwa ni maombi ya kitaifa kuomba Mungu kushusha mvua.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved