logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ushauri wa Betty Kyallo kabla ya kuingia kwenye uhusiano wa kimapenzi

Betty Kyallo alidai kuwa ukiwa ex wa mtu uwe mrembo hata zaidi

image
na

Yanayojiri04 April 2023 - 08:03

Muhtasari


• Mfanyibishara huyo anamiliki kampuni ya flairby Betty ya kutoa huduma ya urembo na bidhaa za urembo.

 

Mjasiriamali Betty Kyalo amewashauri kina dada kabla ya kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi, mwanzo wahakikishe wamejirembesha zaidi.

Kwenye mtandao wake wa Instagram,Betty aliwapa himizo wanaume kuwa  kando na urembo alio nao msichana waangazie nidhamu ya kazi walio nayo malengo yao na ndoto zao na nyoyo zao kubwa.

"Kuwa mpenzi mrembo na hata ex mrembo zaidi," alisema.

"Sahau mwonekano wake, vipi kuhusu maadili yake ya ajabu ya kazi, matamanio yake yaziyozuilika na moyo wake mkubwa wa ajabu," aliongezea Betty.

 

Betty  ni mwanabiashara ambaye amejikuza mwenye biashara ya kuuza  bidhaa za urembo na kutoa huduma za urembo na kampuni yake ya flairby Betty. Amefungua matawi kadhaa ya kampuni hiyo likiwemo la juzi zaidi kule Meru.

Betty ni mwanamke mwenye kujiamini na kujivunia yale aliyofanikisha katika maisha.

Hivi majuzi wakati wa mahojiano na mwanasiasa maarufu Phelix Odiwuor almaarufu Jalang'o, Betty alizungumza kuhusu mapenzi na uhusiano, biashara, uhalisia, na jinsi walivyofichua kuwa kwa sasa wanafanyia kazi Kyallo Kulture msimu wa 2.

Mfanyibiashara huyo alifichua kuwa amekuwa akichumbiana kwa karibu mwaka mmoja na amekuwa akiweka uhusiano wake kuwa wa faragha kwani wakati huu anataka kufanya mambo tofauti na kuona jinsi mambo yatakavyokuwa.

Hapo awali Betty alipoulizwa ni kwanini amekuwa akihamisha biashara yake kutoka eneo moja hadi lingine, mfanyibiashara huyo mwenye umri wa miaka 34 alisema kuwa anapenda miradi mipya na anapenda kuwapa wateja wake fursa na uzoefu wa ajabu na kuongeza kuwa mabadiliko ni mara kwa mara.

Alibainisha kuwa, "Nikipata eneo si zuri kwa wateja wangu, sina tatizo la kuhama na kuongeza kuwa mabadiliko ni ya mara kwa mara ikiwa unaona kitu hakifanyi kazi, unahitaji tu kuhama na kuanza upya." Pia alisema kuwa eneo jipya ni la uboreshaji na anafurahi sana kuanza safari yake mpya.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved