logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ukiwa tajiri, kila msichana atataka hela kutoka kwako na si mapenzi - Diamond Platnumz

Licha ya hivo, Diamond alisisitiza kwa watoto wa kiume kutadfuta hela.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri14 April 2023 - 04:44

Muhtasari


• “Mfanyie mambo Zaidi ya milioni, ya kumfurahisha. Lakini sasa wewe pata tatizo la mkwamo kidogo kifedha, atakuonesha rangi za tabia yake halisi,” Diamond alisema.

Diamond ashauri wanaume kutaduta hela.

Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Wasafi Diamond Platnumz kwa mara nyingine tena amesisitiza watoto wa kiume kwamba kuna haja na kutafuta pesa kwanza kabla ya mapenzi.

Hata hivyo, Simba, kama anavyojiita, amesema kuwa kupata pesa na utajiri si njia mwafaka ya kutarajia mapenzi ya kweli, akidai kuwa kuna changamoto nyingi katka upata penzi la kweli ukiwa unanukia utajiri.

“Pindi tu baada ya kuwa tajiri, kila msichana utakayekutana naye atataka pesa zako na wala sio mapenzi yake ya kweli,” Platnumz alisema.

Platnumz anahisi kwamba wanawake ni viumbe wa ajabu sana ambao kuwaelewa ni kibarua cha kujaribu kupasua jabali ili kupata maji.

Msanii huyo anayetajwa kuwa namba mbili ukanda wa Afrka Mashariki katika utajiri, kulingana na orodha ya Forbes ya mwaka huu alisema kwamba mwanamke ni mtu unayeweza kujitoa kwake kwa asilimia mia ukimfanyia kila kitu lakini mwisho wa siku ukikwamba kidogo tu kifedha, basi ndio naye anakupiga teke.

“Mfanyie mambo Zaidi ya milioni, ya kumfurahisha. Lakini sasa wewe pata tatizo la mkwamo kidogo kifedha, atakuonesha rangi za tabia yake halisi,” Diamond alisema.

Hata hivyo, msanii huyo alisisitiza kuwa watu watafute hela akisema kuwa maisha ya kisasa huwezi kufanikisha jambo lolote pasi na pesa.

Diamond katika siku za hivi karibuni amekuwa gumzo mitandaoni baada ya kuonekana kanisani siku ya Pasaka, wakati wengi wanamjua kama Muislamu anayefunga mwezi mtukufu wa Ramadhan.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved