logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ronaldo afutilia mbali uvumi wa kuachana na mkewe Georgina, "Mapenzi bado yapo!"

Ronaldo alipakia picha wakiwa na mkewe wakikulana mabusu na kugonga cheers kwa glasi za juisi.

image
na Radio Jambo

Makala01 May 2023 - 08:18

Muhtasari


• Picha hiyo ilionekana kuosha kabisa uvumi huo wote ambao ulikuwa unadai kwamba Georgina hana raha na mamake Ronaldo na muda mwingi hukaa kwenye duka lake huko Saudia.

Staa wa soka kutoka Ureno Christiano Ronaldo ameibuka na kufutilia mbali uvumi ulioibuliwa na wanahabari wa michezo nchini Ureno kwamba uhusiano wa mkewe Georgina Rodriguez na mamake Ronaldo umezorota.

Uvumi huo uliibuka katika kipindi cha mazungumzo cha kituo cha runinga cha CMTV cha Ureno Noite das Estrelas, ambapo mwandishi wa habari Quintino Aires, rafiki wa karibu wa mama wa Ronaldo, alidai kuwa tabia za mwanasoka huyo zilionyesha kwamba hakuwa na furaha katika maisha yake ya kibinafsi.

"Haishi wakati wa furaha, na kadiri anavyosonga mbali na mama yake, ndivyo anavyopungua. Na sote tunajua kwa nini anazidi kuwa mbali na familia yake,” Aires alisema, akimnyooshea kidole mpenzi wa Ronaldo, Georgina Rodriguez.

Lakini Ronaldo ambaye hajawahi kulizingumzia hilo alifutilia mbali madai hayo kwa picha ya pamoja wakipigana mabusu na mkewe huku wakigonga cheers ya glasi za juisi na kuweka maneno mawili;

“Cheers kwa mapenzi!”

Picha hiyo ilionekana kuosha kabisa uvumi huo wote ambao ulikuwa unadai kwamba Georgina hana raha na mamake Ronaldo na muda mwingi hukaa kwenye duka lake huko Saudia.

"Georgina hutumia siku yake katika duka la jumla huko Riyadh, na hiyo ndiyo sababu mojawapo kwa nini Cristiano hafurahishwi na hadithi hii," aliongeza mwanahabari huyo aliyekuja na uvumi huo.

Ronaldo na mkewe walikutana mwaka 2016 ambapo wamekuwa wakiishi pamoja kama wanandoa licha ya kutofunga harusi halali.

Mapema mwaka huu, Ronaldo na Georgina waliweka rekodi ya kuwa watu wa kwanza kuruhusiwa kuishi nchini Saudi Arabia bila kuoana rasmi, kwani sheria za Kiislamu katika taifa hilo zinasema kwamba hakuna watu wanaoruhusiwa kuishi kama wanandoa pasi na kuoana rasmi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved