logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Colonel Mustafa afunguka kuhusu video yake akifanya mjengo

Rapa huyo aliambia Mpasho kuwa sio video ya muziki kama inavyodaiwa.

image
na

Yanayojiri04 May 2023 - 12:26

Muhtasari


• "Unapofanya kazi kuna maswala mengi, kunakuwa na beef pia na stori mingi kwa mjengo, kwa hiyo labda kuna mtu aliivujisha,".

Msanii mkongwe kutoka Ogopa Djs, Coonel Mustafa

Rapa aliyegeuka mwigizaji Colonel Mustapha amevunja ukimya saa chache baada ya video yake akifanya kazi kwenye mjengo kuvuja mtandaoni.

Katika mahojiano maalum na Mpasho, Mustapha alithibitisha kuwa video hiyo ni ya kweli na alipatwa na wakati mgumu na kuamua kufanya kazi za ujenzi.

Rapa huyo aliambia Mpasho kuwa sio video ya muziki kama inavyodaiwa.

"Unapofanya kazi kuna maswala mengi, kunakuwa na beef pia na stori mingi kwa mjengo, kwa hiyo labda kuna mtu aliivujisha,".

Hi maze ni blunder, ni blunder," alieleza kuhusu aliyevujisha video hiyo.

"Baada ya habari hiyo kuvuja, nimeshindwa hata kutembea, kwani huwezi jitafutia, sasa itakuwa aje? Na siko vizuri hivo, mambo ni ngumu bana" alisema.

"Kuna kitu nilikuwa nakifanya siwezi kukizungumzia sana, lakini ni shughuli nimekuwa nikifanya kwa mwaka mmoja uliopita"

"Lakini sasa kuna msee tu hapo nadhani ni hivo kuna mtu alivujisha sikujua usiku ndio nilipata taarifa vile nimerudi"

Mustapha alielezea maisha yake kuwa magumu kwa muda. "Mambo yamekuwa magumu hapo nyumbani," alishiriki kwa ufupi.

Aliambia kwamba atazungumza zaidi juu ya safari yake ngumu baadaye.

Ameeleza hayo na rafiki yake "Unajua mafriends nimekuwa nawaambia, hawaskii" aliendelea kuongeza kuwa hakufanya tamasha lolote linalosababisha migogoro ya kifedha.

"Mara ya mwisho kutumbuiza ilikuwa nadhani mwaka jana Aprili hivyo kumekuwa mtu wangu," alikiri.

Alianza kazi za ujenzi ili kujiruzuku badala ya kuomba msaada wa umma.

"Hiyo kazi ni ngumu, inabidi saa zingine at least hata nimejaribu sana mwaka mmoja, kama ningeomba nimeomba kwa simu wangekuwa wame screenshot," alisema.

Mustapha pia alikiri kwamba mama yake ni mgonjwa na mahitaji yake ya matibabu ni ghali. Anafanyiwa chemotherapy.

"Hii kitu amekuwa nayo kwa muda wa miezi 8. Ni kichaa, mimi mwenyewe imekuwa noma,"


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved