logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Baada ya Davido na mkewe, Don Jazzy naye apagawa na Single Again ya Harmonize

Don Jazz yalikuwa anajitania kwa nini yuko single haswa baada ya Rihanna kuolewa.

image
na Radio Jambo

Habari08 May 2023 - 04:35

Muhtasari


• “Sawa acha tujaribu hi tena, mbona niko singo?” Jazzy aliandika kwenye video hiyo, "ni kwa sabau sitaki kujukumika,"

Harmonize mawinguni Don Jazzy akishiriki Single Again

Baada ya msanii maarufu Afrika, Davido na mkewe kuonesha wazi wazi mapenzi yao kwa wimbo wa Single Again kutoka kwa mkurugenzi mtendaji wa lebo ya Konde Music Worldwide, mkurugenzi mkuu mtendaji wa lebo maarufu ya muziki Marvin Records, Don Jazzy naye pia ameupa shafu wimbo huo.

Jazzy kupitia ukurasa wake wa TikTok alipakia video mbili akiwa anaimba wimbo huo wa Harmonize kama njia moja ya kuonesha kuukubali kupita maelezo.

Don Jazzy alipakia wimbo huo akitania kwamba yuko singo baada ya msanii Rihanna ambaye alitajwa kuwa anampenda sana kuolewa na rapper Asap Rocky.

“Sawa acha tujaribu hi tena, mbona niko singo?” Jazzy aliandika kwenye video hiyo, "ni kwa sabau sitaki kujukumika,"

 Hata hivyo, akiwa na furaha kubwa, Harmonize alishiriki kipande hicho cha video kwenye Instagram yake akisema kuwa kumepambazuka upande wake kwani CEO wa lebo kubwa Zaidi duniani aliweza kuufikia wimbo wake na kuupenda miongoni mwa mamilioni ya ngoma nzuri ambazo zipo pale nje kwenye soko.

Konde alimliwaza Jazzy akimwambia kuwa atamtafutia Rihanna mwingine kutoka Tanzania ili kuhakikisha kwamba hatokuwa singo tena.

“Mabibi na mabwana bosi mkubwa Don Jazzy hayuko tayari kujukumika baada ya Asap Rocky kumchukua Rihanna. Usiwe na shaka baba Jazzy, nitahakikisha umepata Rihanna mwingine kutoka Tanzania ili usiwe singo tena,” Harmonize aliandika.

Baadhi ya wachambuzi wa tasnia ya burudani walihisi kwamba hii ndio fursa ya kipekee ambayo imemtokea Harmonize machoni na hafai kuiacha ipotee kwani kupitia kwa Jazzy, kuna uwezo mkubwa sana wa kumpata msanii mkubwa wa Marvin Records atakayedandia kwenye remix ya Single Again na kuifanya kuwa kubwa kuliko.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved