logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Samidoh avunja kimya baada ya mkewe kupakia picha akiwa na mwanajeshi wa Marekani

Nyamu hajamuonea huruma mama wa watoto watatu

image
na Radio Jambo

Makala10 May 2023 - 12:11

Muhtasari


  • Wanamitandao wengi walidai kana kwamba anamkejeli mkewe kwa methali hiyo inayotoka au kusemwa na watu wa loitoktok.

Saa chache baada ya mkewe kupakia picha kwenye mtandao wake wa kijamii akiwa na mwanajeshi wa Marekani, mwimbaji wa Mugithi Sammy Muchoki almaarufu Samidoh amevunja ukimya kwenye mitandao yake ya kijamii.

Wanamitandao wengi walidai kana kwamba anamkejeli mkewe kwa methali hiyo inayotoka au kusemwa na watu wa loitoktok.

''Mwanamke anayeruhusu watu kuonja chakula chake kabla ya kununua huishia kulisha kijiji kizima bila kuuza sahani ~ Kimana -Methali ya Loitoktok,'' Samidoh alichapisha.

Edday Nderitu saa chache zilizopita alioakiapicha akiwa na mwanajeshi wa Marekani ambaye hakufahamika jina lake huku picha hiyo ikisambaa mitandaoni na wengi wakimpongeza wakimtaka kutafuta mapenzi nje ya nchi.

Edday na Samidoh wamekuwa na matatizo ya ndoa baada ya mwimbaji huyo kuhusika na seneta mteule Karen Nyamu akiwa na watoto wawili naye.

Nyamu hajamuonea huruma mama wa watoto watatu. Amekuwa akianika uhusiano wake na msanii Mugithi.

Edday, ambaye anafurahia likizo na watoto wake katika nchi hiyo ya Magharibi, alishiriki picha hiyo huku akiwasalimu mashabiki wake.

Baadhi ya wanamitandao walionekana wakimshauri mama huyo wa watoto watatu kumtema Samidoh na kubaki na mwanajeshi huyo.

Wengine walidai kuwa Edday ana ladha ya wanaume waliovalia sare kwani mbali na muziki, Samidoh pia ni afisa wa polisi.

Mwaka jana, mwimbaji huyo wa Mugithi ambaye ni afisa wa Polisi wa Utawala alisema hajapata sababu ya kuacha kazi ya polisi licha ya mafanikio yake katika tasnia ya muziki. Mara nyingi yeye hushiriki picha na video zake akitumbuiza katika sehemu mbalimbali za dunia lakini si akitoa huduma za afisa wa polisi.

"Ninafanya kazi siku za wiki na inapohitajika pamoja na kipindi cha wikendi huwa nafanya muziki wangu, kama talanta nyingine yoyote katika huduma ya polisi," alisema katika mahojiana na Word Is.

 

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved