logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jaguar aibua maswali akionekana na mrembo, helikopta na magari ya kifahari

Baadhi walihisi ni video ya wimbo mpya ambayo alikuwa anamshirikisha kama vixen.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri11 May 2023 - 06:00

Muhtasari


• Nyuma yao, kulikuwa na magari mawili ya kifahari na mezani chupa na bilauri zilizomiminiwa vinywaji hivyo ghali.

Jaguar akipunja maisha na mrembo asiyejulikana.

Msanii mkongwe kutoka nchini Kenya Charles Njagua Kanyi almaarufu Jaguar amezua maswali mengi kuliko majibu mitandaoni baada ya kuonekana akila bata katika sehemu ya mikutano ya faragha na mrembo asiyetambulika lakini pia na vitu vya thamani kama magari vinywaji bila kusahau ndege aina ya helikopta.

Katika picha hizo tatu ambapo Jaguar alizichapisha kwenye kurasa zake mitandaoni, ya kwanza ilimuonesha akitembea na mrembo huyo kutoka kwa helikopta, huku wameshikana mikono wakiongozana kwenda katika meza iliyokuwa imeandaliwa na vyakula vya aina mbalimbali.

Picha ya pili na ya tatu ziliwaonyesha wawili hao wameketi mezani mkabala kutoka kwa kila mmoja wakifanya mazungumza huku meza ikiwa imefunikwa na vinywaji na nyuma yao kulikuwa na magari mawili ya kifahari.

Jaguar hakutoa ufafanuzi wowote kuhusu matukio katika picha hizo bali aliandika kapsheni kama ya kutoa himizo hivi akiwashauri wafuasi na mashabiki wake kutokengeushwa na kitu chochote na badala yake kubaki katika uhalisia wao tu.

“Hakuna mtu anayeweza kuwa wewe bora kuliko wewe mwenyewe,” Jaguar aliandika.

Hata hivyo, picha hizo ziliibua maswali mengi, watu wakishindwa kumtambua kwa mara moja mrembo huyo alikuwa nani, kwani inafahamika Jaguar ni baba mwenye familia ya watoto watatu na huwa hapendi kupakia mambo ya kifamilia mitandaoni.

Wengine pia walihisi Jaguar ni kama amerejea kwenye muziki na ni sehemu ya video ya wimbo wake ambapo alikuwa anamshirikisha mrembo huyo kama vixen.

Na wengine waliibuka na dhana kwamba helikopta ile ni ya mwandani wake rais William Ruto ,kwani ilishabihiana kwa sehemu kubwa na yake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved