logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Pierra Makena atoa onyo kali kwa watu wanaoiga wazo lake la Park & Chill

Makena alisema kuna baadhi ya makundi ya watu ambao wanategemea ubunifu wake.

image
na

Habari11 May 2023 - 05:52

Muhtasari


• "Mbona watu wasije na mawazo yao ya kibunifu badala ya kuiga? " Pierra mwenye hasira aliandika kwenye Instastory yake.

Mcheza santuri maarufu wa kike, Pierra Makena ametumia ukurasa wake wa Instagram kwa hasira ya muda mrefu kueleza kusikitishwa kwake na ukosefu wa ubunifu katika tasnia hiyo na watu kuiba dhana yake na kuipitisha kama yao.

Makena mwenye umri wa miaka 42 ambaye pia ni mwigizaji na mfawidhi alishiriki kwamba kuiga na kuchapisha kulionyesha vibaya tasnia ya burudani nchini Kenya na kumwacha na tope usoni.

"Enyewe tasnia yetu imechafuliwa!' Makena alisema.

Aliendelea kuongeza kukerwa kwake na kile anachotaja kama ukosefu wa uhalisia wa watu.

"Mbona watu wasije na mawazo yao ya kibunifu badala ya kuiga? Sasa leo nimeona chill na vibe, jana niliona Park na chew  kisha juzi Park na Vibe... yaani inamaanisha kwamba hivyo ndivyo tulivyo na mawazo finyu?" Pierra mwenye hasira aliandika kwenye Instastory yake.

Mama huyo wa binti mmoja ni maarufu kwa kuongoza tafrija na matamasha kama DJ kwenye Park na Chill ambapo washereheshaji hujitokeza na magari yao na kujivinjari huku wakifurahia ustadi wake katika kupakua burudani

Mama Pokot akionyesha masikitiko yake alitaja kuwa watu hawa walio na nia ya kuchukua wazo lake la ubunifu kama lao wamefikia hatua ya kumfanya atiwe mbaroni kwa sababu walidhani ni mnyonge.

"Halafu unaiga kila kitu ingine.....na kwa sababu unafikiri una mamlaka zaidi unawatafuta wanawake waliopoteza matumaini maishani kwa sababu unafikiri hawawezi kujipigania. Na haswa wacheza santuri wa kiume ambao kila mara wanafanya makusudi kuangusha ushindi wangu....subirini," Makena alicharuka.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved