logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Katibu mwandamizi Charles Njagua adai kuwa tajiri kuliko Akothee na Harmonize

Jagua atishia kutoka ulingo wa muziki ikiwa Akothee na Harmonize wana utajiri kumshinda.

image
na

Habari12 May 2023 - 10:28

Muhtasari


• Jaguar akizungumza na wanahabari kuhusu kibao chake kipya akimshirikisha  msanii wa Tanzania Lava Lava alisema kuwa anamshukuru Mungu kwa utajiri wake.

• Jaguar aliongeza amekuwa katika tasnia ya muziki nchini kwa muda wa zaidi ya miaka 15.

Katibu mwandamizi wa Wizara ya Vijana, Sanaa na Michezo Charles Njagua amesema kuwa ataastaafu kama akothee na Harmonize wana utajiri kumshinda.

Charles Njagua maarufu Jaguar, akizungumza na wanahabari kuhusu kibao chake kipya alichomshirikisha msanii wa Tanzania Lava Lava alisema kuwa anamshukuru Mungu kwa utajiri wake.

“Kuna orodha iliyochapishwa hivi majuzi na ulikuwa nambari ya pili Kenya kama msanii Tajiri zaidi Kenya namba 7 katika wasanii wa Africa Mshariki na ripoti ile ilisema una thamani ya takriban shilingi millioni 958.3, je hiyo ni ukweli?” aliuliza mwanahabari mmoja.

Jaguar alijibu “ unaona Harmonize ako namba sijui ngapi na Akothee ako namba moja, lakini mimi naeza apa kama Harmonize na Akothee wamenishinda kwa utajiri nitaacha mziki leo”

Jaguar aliongeza kuwa amekuwa katika tasnia ya muziki nchini kwa muda wa zaidi ya miaka 15.

Aliwakashifu Akothee na Harmonize kwa kununua magari na mali ili kuonyesha utajiri wao na kusema kuwa yeye amewekeza kwa muda sasa.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved