logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kamwe usimpe mwanaume jukwaa la kukukosea heshima - Akothee awashauri kina dada

"Ikiwa miaka ambayo umejitolea kufikiria kuwa anaweza kubadilika haimwongezi pia. Piga hatua" - Akothee.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri24 May 2023 - 04:10

Muhtasari


• Akothee alishauri kina dada kutonyongonyea mbele ya wanaume ambao wanawaonesha madharau hadharani.

• Msanii huyo mama wa watoto watano alisema mwanamke anayejitambua hawezi kuvumilia manyanyaso kisa ndoa.

Akothee atoa ushauri kwa wanawake wanaonyanyasika kwenye ndoa

Mjasiriamali na mwanamuziki Akothee ambaye kwa muda mrefu alikuwa akijitambulisha kama rais wa kina mama wasio na waume kabla ya kuolewa mwezi jana amerudi tena safari hii akitoa ushauri kwa wanawake wote.

Mama huyo wa tambo nyingi aliwashauri wanawake kutoruhusu hata chembe ya muda na nafasi zao kuwapa wanaume ili kuwapaka dharau.

Akothee aliwataka kina mama kuweka mipaka ya kinachofanywa dhidi yao na kisichostahili ufanywa dhidi yao kuanzia mwanzo kabla mapenzi hayajakolea munyu.

“Kamwe usimpe mwanaume jukwaa la kukukosea heshima. Weka mambo sawa tangu mwanzo mjulishe cha kufanya na kisichofanywa. Wanawake wengi wamevunjika na kuharibiwa na uhusiano ambao haufai uwekezaji wao,” Akothee alitema lulu.

Msanii huyo mama wa watoto watano alisema kuwa hata kama mwanamke umeishi na mwanaume kwa miaka mingi ukiwa na matumaini kwamba atabadilika na haoneshi dalili zozote za kubadilika, usiendelee kuharibu muda wako badala yake jitoe na kuanza maisha yako binafsi.

“Ndio, labda mmeishi pamoja kwa miaka mingi, lakini Madam, Madam, ikiwa miaka ambayo umejitolea kufikiria kuwa anaweza kubadilika haimwongezi pia. Piga hatua, miliki maisha yako na uendelee. Wanadamu wanaweza kuwa wabinafsi sana. Usife mke mwaminifu na maisha matupu,” Akothee alisema.

 Hata hivyo, kabla ya kuzingatia ushauri huu wa Akothee, msanii huyo alitoa tahadhari kubwa akisema kuwa katika harakati za kutoka katika ndoa, mwanzo hakikisha kuwa utakwenda kuhangaika na lazima uwe na pesa zako.

“Lakini kwanza jitayarishe kuchakarika na upate uhuru wa kifedha. Wanawake wengi hawajastahiki Sanaa ya UPATIKANAJI, UDHIBITI NA UMILIKI,” Akothee alimaliza.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved