logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mbosso azungumzia mzozo wake na Marioo

“Mimi kwenye shoo yake hakunialika,au hata kuniposti labda ningeona mwaliko huo," Mbosso alilalamika.

image
na

Habari24 May 2023 - 04:45

Muhtasari


•Kulingana na Mbosso, kila msanii hasa katika Wasafi anapokuwa na jambo au sherehe huwaalika wengine .

•Mbosso aliendelea kusema kuwa,alimkaribisha  Marioo alipokuwa akizindua IP yake.

Msanii wa nyimbo za bongofleva kutoka Tanzania Yusuf Kilungi maarufu Mbosso  amefunguka kuhusu mzozo unaodaiwa kuwepo kati yake na Marioo.

Kulingana naye, kila msanii hasa katika Wasafi anapokuwa na jambo au sherehe huwaalika wengine hivi kwamba iwapo hujaalikwa huwezi kuhudhuria kwa hofu ya kuzuiliwa mlangoni au aibu yoyote ile.

Licha ya wasanii wengi wa Bongo kuhudhuria hafla ya uzinduzi wa albamu ya Marioo mapema mwaka huu, Mbosso hakuonekana pale na katika mahojiano na Wasafi Media aliombwa kueleza kwa nini hakuhudhuria.

“Hivi leo nataka niweke kila kitu sawa.Mimi huwa sina unafiki maana humwaalika kila mtu katika jambo langu na hasa watu wanaotuweka katika picha tofauti, pia huwaalika ndipo waone sisi hatuna shida,”  alisema.

Mbosso aliendelea kusema kuwa,alimkaribisha  Marioo alipokuwa akizindua IP yake, na pia aliposti kwenye ukurasa wake licha ya kuongea naye binafsi, lakini  kwake yeye Marioo hakumjulisha kuwa angekuwa akizindua jambo fulani au albamu mpya.

Mimi kwenye shoo yake hakunialika,au hata kuniposti labda ningeona mwaliko huo kwenye mitandao na kuhudhuria. Kwenye baadhi ya picha zilikuwa na logo, ya Diamond ilikuwa na logo ikiwa na maana ndiye pekee alikuwa amelikwa” Alisisitiza kuhusu kutohudhuria kwake.

Mbosso anayeendelea kushamiri kutokana na mdundo wa nyimbo zake  alitia sahihi na shirika kuu Afrika la kurekodi  nyimbo WCB Wasafi tangu mwaka wa 2017 kuendeleza kipaji chake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved