logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamume wangu akiacha kunitumia pesa nitamuacha bila kufikiria mara mbili - Jackie Matubia

Matubia kwa sasa wanakisiwa kutokuwa katika hali sawa na mpenzi wake Blessing Lunga'ho.

image
na Radio Jambo

Habari24 May 2023 - 05:05

Muhtasari


• Matubia na mpenzi wake Blessing Lung'aho wamekuwa wakisemekana kutokuwa na maelewano katika siku za hivi karibuni.

• Wenzi hao walianza kuchumbiana mnamo Februari 2021 na hivi majuzi walisherehekea kumbukumbu yao ya pili.

Wapenzi waigizaji Lungaho na Matubia

Mwigizaji Jackie Matubia amedai kuwa yeye hawezi kuendelea katka uhusiano na mwanamume ambaye ameacha kumtumia hela za matunzo na matumizi mengine.

Mwigizaji huyo katika klipu aliyoipakia kwenye Tiktok yake akiiga sauti ya mwanamke mwingine, alisema kuwa hawezi hata fikiria mara mbili kuhusu hatima ya uhusiano wake na mwanamume wake, ikiwa mwanamume huyo ataweka kikomo katika kumpa hela.

“Nitamuacha mapema mapema, nitamblock na kusema kweli siwezi kuwa na biashara yoyote na mtu ambaye hataki kutumia pesa zake kwangu. Ni rahisi kama ABC…” Jackie Matubia aliiga sauti hiyo.

Kwa muda wa wiki kadhaa sasa, Matubia na mpenzi wake Blessing Lung’aho wamekuwa wakisemekana kutokuwa katika hali sawa, mashabiki wao wakihisi kuwa huenda wawili hao wameachana kinyemela.

Hata hivyo, Matubia katika mahojiano ya kipekee na kituo kimoja cha redio humu nchini alifutilia mbali uvumi huo akisema kuwa wako sawa na Lung’aho lakini pia alionekana kutotaka kuzungumzia mengi kwa kina kuhusu hali ya uhusiano wao.

Mashabiki walianza kuhisi mambo si shwari katika uhusiano wao baada ya Matubia kupakia klipu kwenye Tiktok yake akiiga sauti ya mtu ambaye alikuwa ameulizwa uhakika kuhusu uhusiano wake wa kimapenzi na kusema kuwa hakuwa na uhakika wowote kuhusu mapenzi.

Katika video hii, alizungumza kuhusu kosa alilofanya na jinsi ambavyo hangeweza kupona kutokana nalo.

“Nilikuwa nafikirianga ni mimi pekee yangu huwa naitwa babyghurl na nikafanya makosa nikashika simu yake,” Matubia alidokeza kiini cha uvumi wa kuachana kwao.

Wenzi hao walianza kuchumbiana mnamo Februari 2021 na hivi majuzi walisherehekea kumbukumbu yao ya pili.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved