logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rapa maarufu amtumia babake Diamond kama 'video king' kwenye wimbo wake

Baadhi walihisi wimbo huo ulikuwa unapiga mafamba uhusiano wa Diamond kwa babake.

image
na Radio Jambo

Habari24 May 2023 - 05:09

Muhtasari


• Katika video hiyo, Mzee Abdul anaonekana akijitahidi kuilisha familia yake ambaye ni mke wake na mtoto wake wa kiume.

• Baadae mtoto anapokuwa mkubwa anamkataa babake na kumpa mama thamani yote akisema baba hana maana tena.

Mzee Abdul aigiza kama video king kwenye ngoma ya mpinzani wa Diamond.

Msanii rapa wa Bongo Fleva Nay wa Mitego ameachia kazi mpya akimshirikisha msanii Linah Sanga na tayari video ya ngoma hiyo kwa jina ‘Mshua’ imepakiwa YouTube.

Video hiyo imegeuka kuwa gumzo kubwa haswa baada ya baba yake na Diamond Platnumz, Mzee Abdul akiigiza kama ‘video King’ – jambo ambalo limewaacha wengi wakizungumza maana ya Nay kumtumia mzee wa Diamond kwenye video yake.

Kwa muda mrefu mzee Abdul alikuwa anafahamika na wengi kama babake Diamond kabla ya miaka ya hivi karibuni mama Dangote kuweka wazi kuwa siye baba wa kumzaa Diamond, akijaribu kuteua kitendawili kuhusu ni kwa nini msanii huyo licha ya kunukia utajiri hajawahi msaidia mzee huyo.

Mzee huyo aliwahi fanya mahojiano akisema kuwa anaugua saratani ya ngozi lakini hakuna mtu kutoka kwa wale aliokuwa akiwaita familia yake – kwa maana ya mama Dangote na mwanawe Diamond, hawakuwahi kumpa msaada wowote.

Kilichoibua gumzo pevu kuhusu video hiyo hata hivyo ni mada na maana ya wimbo huo ambao umejikita Zaidi katika kuzungumzia mateso na shida ambazo baba anapitia kuhakikisha kwamba familia yake iko sawa kwa kila kitu lakini mwisho wa siku anageuzwa kuwa zulia la kukanyagwa tu.

“Kwenye familia wewe ndio kichwa na tuliona ulivyopambana lakini mimi na wadogo zangu tulisema hivi nani kama mama,” sehemu ya mishororo kwenye shairi hilo la Nay wa Mitego iliimba.

Sasa hiki ndicho kimewafanya baadhi wahisi kwamba Nay alikuwa anatupa bomu la moto kwa Diamond na mama yake kwa kumtelekeza mzee wake licha ya kujitoa pakubwa kiasi msanii huyo alikuwa mdogo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved