Fahari ya mama: Beyonce afurahia kutumbuiza kwenye jukwaa moja na bintiye, 11

'Mzaliwa wangu wa kwanza mzuri. Ninajivunia na ninashukuru kuwa mama yako. Unatuletea furaha nyingi, malaika wangu mtamu.'

Muhtasari

• Picha ya kwanza ilionyesha Blue akiwa amesimama kuelekea mbele ya jukwaa huku mama yake akiwa nyuma yake.

• Mshindi wa Grammy kisha alipakia klipu fupi ya mwendo wa polepole iliyoonyesha mtoto wake mkubwa akiwaongoza wacheza densi jukwaani.

Beyonce afurahia kushiriki jukwaa moja la utumbuizaji na binti yake mwenye umri wa miaka 11.
Beyonce afurahia kushiriki jukwaa moja la utumbuizaji na binti yake mwenye umri wa miaka 11.
Image: Instagram

Beyonce alikuwa mama 'mwenye fahari' aliposhiriki video maalum ya Instagram Jumatatu baada ya bintiye, Blue Ivy, kujiunga naye kwenye jukwaa na kutumbuiza pamoja katika ziara yake ya muziki ya Renaissance huko Paris.

Hitmaker wa The Crazy In Love, 41, ambaye aliwashangaza mashabiki kwenye umati siku ya Ijumaa alipomtoa mtoto wake mkubwa, aliimba nyimbo mbili za My Power na Black Parade huku kijana huyo wa miaka 11 akiungana na wanadansi wengine kutumbuiza.

Mwimbaji huyo, ambaye anashiriki Blue pamoja na mapacha Rumi na Sir, 5, na mumewe Jay-Z, walipakia picha na klipu zote kwenye chapisho ili kuadhimisha usiku huo maalum.

Katika nukuu, mama wa watoto watatu aliandika kwa utamu, 'Mzaliwa wangu wa kwanza mzuri. Ninajivunia na ninashukuru kuwa mama yako. Unatuletea furaha nyingi, malaika wangu mtamu.'

Picha ya kwanza ilionyesha Blue akiwa amesimama kuelekea mbele ya jukwaa huku mama yake akiwa nyuma yake moja kwa moja. Alivalia suti ya rangi ya fedha, inayometa pamoja na suruali ya kumeta, iliyofanana na jukwaa la Beyonce.

Mshindi wa Grammy kisha alipakia klipu fupi ya mwendo wa polepole iliyoonyesha mtoto wake mkubwa akiwaongoza wacheza densi wengine walipoanza kucheza kwa choreography.

Beyonce alionekana amesimama kwenye gari nyuma huku akiimba nyimbo chache kwa hadhira iliyosisimka.

Reel fupi ya mwisho ilionyesha Bluu akionekana kwenye fremu ya kamera na kuachia tabasamu la haraka kabla ya kuruka tena kwenye utaratibu wa kucheza jukwaani.

Wakati wa mahojiano ya awali na Vogue, mwimbaji wa Partition alisema kwamba binti yake mkubwa "ni mwerevu sana" na baadaye akaeleza, "Ninapomwambia kuwa ninajivunia yeye, ananiambia kuwa anajivunia mimi na kwamba ninafanya kazi nzuri.'

'Ni utamu kupita kiasi. Anayeyusha moyo wangu. Ninaamini njia bora ya kuwafundisha ni kuwa kielelezo,' aliongeza, akiwarejelea watoto wake wote.

Beyonce si msanii wa kwanza kutumbuiza na bintiye kwenye jukwaa moja.

Nchini Kenya, TikToker Michael Bundi kwa Zaidi ya mwaka mmoja sasa amekuwa akiwakosha mashabiki wake kwa kufanya maigizo ya nyimbo za wasanii wengine pamoja, wakiimba kama watu wako studioni kurekodi nyimbo – yeye pamoja na mvulana wake mdogo, Fayez.

Pia mwezi Janauri, Mkenya Richard Bett anayeishi Marekani aligonga vichwa vya habari baada ya klipu kuenezwa akionekana kuimba na binti yake mdogo Aiko Bett, klipu iliyomvutia mwimbaji mkongwe na muongozaji wa kipindi Kelly Clarkson kuwapa mwaliko na kutumbuiza moja kwa moja kwenye shoo yake.