Siwezi toka Wasafi-Meneja wa Diamond adokeza njia pekee ya kuondoka Wasafi

Aliapa kuwa yuko tayari kupoteza mguu katika harakati za kuweka kazi yake Wasafi.

Muhtasari
  • Akizungumza na kipindi maarufu cha redio nchini Tanzania, meneja huyo alifichua kuwa hatawahi kuacha lebo hiyo ya muziki.
  • Hata hivyo, alidai kuwa kwenye kazi zao wamekuwa wakinyanyaswa na mashabiki na kwa sasa wanavuna matunda ya bidii yao.
Image: INSTAGRAM// BABU TALE

Mmoja wa mameneja watatu wanaoshughulikia biashara za Diamond Platnumz Babu Tale amefichua njia pekee ya mwimbaji huyo kumuondoa kwenye Lebo ya Wasafi Record.

Akizungumza na kipindi maarufu cha redio nchini Tanzania, meneja huyo alifichua kuwa hatawahi kuacha lebo hiyo ya muziki.

Alidokeza kwamba walikuwa wakihangaika pamoja kabla ya kupata mafanikio na kamwe hataruhusu hilo kuteleza kwa urahisi.

Hata hivyo, alidai kuwa kwenye kazi zao wamekuwa wakinyanyaswa na mashabiki na kwa sasa wanavuna matunda ya bidii yao.

Pia alidokeza kuwa hawawezi kutengana kutokana na hali ya uhusiano wao na kumkata kwenye lebo hiyo itakuwa balaa.

Aliapa kuwa yuko tayari kupoteza mguu katika harakati za kuweka kazi yake Wasafi.

"Siku yenye msanii Diamond ataniambia hanitaki wasafi atanikata mguu,siwezi toka Wasafi,"Tale alidokeza.

Wiki iliyopita akiwa kwenye mahojiano alitoa maelezo kuhusu ni kwa nini msanii Diamond anawapa wasanii wapya mikataba ya miaka mitano hadi 10.

Katika mahojiano na Millard Ayo, Tale alifichua kwamba wasanii wapya ambao wamesainiwa katika lebo ya WCB Wasafi tangu uzinduzi wake, wote hawakupewa mkataba unaozidi miaka 10, na kuelezea ni kwa nini.

Mwanzo, Tale alianza kwa kuzungumza ni kwa nini Platnumz amechukua muda mrefu kuwasaini wasanii wengine ili kuchukua nafasi ya wale walioondoka akiwemo Rich Mavoko, Harmonize na Rayvanny.

“Kumpa msanii mkataba ni hatua. Diamond anachunguza vitu vingi sana. Kuondoka kwa wasanii kulitupatia hofu zile za kuangalia huyu, aah huyu… tulikuwa tunasaini haraka unajua lakini tuliingia hofu.. huyu… ile hipo ile kama binadamu,” Tale alisema.