logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mmiliki wa jumba alikoishi AKA atoa notisi kwa familia kuondoa vitu vyake, kumbe halikuwa lake!

Hii licha ya AKA, mzaliwa wa Kiernan Forbes, kudaiwa kulipa kodi yake mapema hadi Septemba mwaka huu.

image
na Radio Jambo

Makala14 June 2023 - 09:09

Muhtasari


• Miongoni mwa magari yaliyokuwa yakiendeshwa na Supastaa huyo, ni BMW i8 yenye thamani ya angalau R2-milioni (Ksh 15m).

• Pia alimiliki BMW X7 yenye thamani ya zaidi ya R2.6-milioni (Ksh 19.6m) alizonunua muda mfupi kabla ya kifo chake.

Nyumba aliyokuwa akiishi AKA yawekwa sokoni na mwenye nyumba halisi licha ya wengi kudhani nyumba hiyo ilikuwa inamilikiwa na msanii huyo.

Siku mbili zilizopita, kuliibuka na taarifa zenye ukakasi kwamba mmiliki wa jumba alikokuwa anaishi msanii marehemu wa Afrika Kusini AKA ametoa notisi kwa familia yake kuondoa vitu vyote vya msanii huyo huku akitaka kulipiga mnada sokoni.

Taarifa hizi ziliwaacha wengi vinywa wazi, kwani walikuwa wanajua jumba hilo la kifahari lilikuwa la msanii huyo kumbe alikuwa tu mpangaji.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari, AKA alikuwa analipia kodi ya randi za Afrika Kusini elfu 30 kwa kila mwezi sawa na shilingi laki mbili na elfu 25 za Kenya.

Jarida la Sunday World la nchini Afrika Kusini liliripoti kwamba mmiliki wa jumba hilo la kifahari alitoa notisi hiyo baada ya kukatisha mkataba wa AKA miezi michache tu baada ya kifo chake.

“Haikuwa nyumba yake. Alikuwa akikodisha nyumba hiyo na alikuwa akilipa takriban R40 000 kwa mwezi. Najua watu walidhani hii ilikuwa nyumba yake kwa sababu ya magari aliyokuwa akiendesha,” alisema mshirika wa karibu wa AKA, ambaye hakutaka jina lake litajwe kwa hofu ya kudhulumiwa, kulingana na jarida hio.

Miongoni mwa magari yaliyokuwa yakiendeshwa na Supastaa huyo, ni BMW i8 yenye thamani ya angalau R2-milioni (Ksh 15m) na BMW X7 yenye thamani ya zaidi ya R2.6-milioni (Ksh 19.6m) alizonunua muda mfupi kabla ya kifo chake.

Mshirika huyo alisema Mekoa, mmiliki wa jumba, aliiambia familia ya AKA kuwa alikuwa amekatisha makubaliano ya kukodisha na kuwataka waende kwenye jumba hilo na kuchukua mali yake.

"Walizikusanya na inaonekana kuzifungia kwenye hifadhi," mshirika huyo alisema.

Hii licha ya AKA, mzaliwa wa Kiernan Forbes, kudaiwa kulipa kodi yake mapema hadi Septemba mwaka huu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved