logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Binti wa rais Charlene Ruto alia kushambuliwa na nyuki

Walikuwa na asali nzuri. - Charlene Ruto.

image
na Radio Jambo

Habari02 July 2023 - 09:15

Muhtasari


• “Kati ya Jumanne na Jumatano nilitembelea mizinga ya nyuki ya babu yangu ili kusaidia kusafisha na kuvuna asali yao" - Charlene.

Charlene Ruto afichua sababu ya kuita mzinga Bottom Up.

Binti wa kwanza wa taifa, Charlene Ruto ambaye ni mkulima hodari wa nyuki amelia kwamba mapema wiki jana alipotembelea shamba la nyuki la babu yake alishambuliwa na nyuki na kumuuma mara tatu.

Charlene alipakia rundo la picha na video kwenye Twitter yake akitoa maelezo mafupi kwa kila picha na video ambapo alisema kuwa nyuki walimuuma mara tatu baada ya zipu ya wanda lake la kujikinga dhidi ya mishale ya nyuki kukataa kufungika yote.

“Kati ya Jumanne na Jumatano nilitembelea mizinga ya nyuki ya babu yangu ili kusaidia kusafisha na kuvuna asali yao. Walikuwa na asali nzuri. Siku ya Jumatano niliumwa mara tatu kwa sababu zipu ya suti yangu haikufika mwisho (hatuwezi kamwe kuzungumzia usalama na tahadhari zinazohitajika katika ufugaji nyuki),” Charlene alisema.

Hata hivyo baada ya kuumwa na nyuki, binti wa kwanza wa taifa alijitapa akisema kwamba hakupata uvimbe unaosababishwa na mishale mikali ya nyuki, huku akisema kuwa shughuli ziliendelea kama kawaida.

“Uzuri sikufura sana😅 Hatukuvuna asali hii kwa sababu bar hiyo inatoka kwenye Brood box... imekaguliwa na kurudishwa...iko na nyuki wanaokuja,” Binti Ruto alisema.

Binti huyo wa kwanza amekuwa akijitahidi sana katika ukulima wa kufuga nyuki ambapo mwezi Aprili alilazimika kuhadithia jinsi alivyoafikia uamuzi wa kuita mzinga mmoja kwa jina la Bottom Up, kauli mbiu ambayo inahusishwa na sera za kisiasa za babake, rais Ruto.

“Tulipokuwa tukifanya ukaguzi kwenye mizinga, tuligundua kuwa baadhi ya nyuki walikuwa wamevamia mzinga ambao ulikuwa umetegwa kichwa chini na kuanza kutengeneza masega ya asali. Tuligeuza mzinga kuwa wima, tukavuna asali iliyopo na kuupa jina la "Bottom Up" kwa uchunguzi rahisi wa maendeleo yake,” Charlene alifafanua.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved